Careen minde

Careen minde I am model,dancer,red cross volunteer, BICT student and medical laboratorian

15/06/2019

Beautiful kilimanjaro 😍
15/06/2019

Beautiful kilimanjaro 😍

10/06/2019
Lav es bell😍
19/05/2019

Lav es bell😍

17/05/2019
27/08/2015

Vijana Huuliza . . .
Je, Vijana Wenzako Wanaweza Kukuathiri Sana?
“Mimi sifikiri kwamba ninaathiriwa na vijana
wenzangu.” —Pamela, mwanafunzi wa shule ya
sekondari.
“Nadhani kwamba sasa siathiriwi tena na vijana
wenzangu. Mimi mwenyewe ndiye
ninayejiongoza.”—Robbie, mwanamume kijana.
JE, UMEWAHI kuhisi hivyo? Naam, huenda
unajua kwamba Biblia inasema: “Mashirika
mabaya huharibu mazoea yenye mafaa.” ( 1
Wakorintho 15:33 ) Lakini, huenda bado ukajiuliza
hivi, ‘Je, kweli uvutano wa marika ni wenye
nguvu sana k**a vile wazazi wangu na watu
wazima wengine wanavyosema?’
Iwapo wewe hujiuliza hivyo mara kwa mara,
kumbuka kwamba vijana wengine pia hujiuliza
swali hilo. Lakini tunakuomba uchunguze jambo
hili. Je, inawezekana kwamba mtu aathiriwe sana
na marika wake? Vijana wengi wameshangaa
wanapotambua jinsi ambavyo wameathiriwa sana
na marika wao. Kwa mfano, Angie anakubali
kwamba anafanya juu chini ili apendwe na watu.
Anasema hivi: “Nyakati nyingine uvutano wa
marafiki unaweza kuwa wenye nguvu sana kiasi
cha kumfanya mtu asitambue kuwa anaathiriwa
na marika wake. Unaweza kufikiri kwamba ni
wewe mwenyewe unayejiongoza kufanya
mambo.”
Vivyo hivyo, Robbie, aliyenukuliwa hapo juu,
anasema kwamba yeye hasa ndiye
anayejiongoza. Hata hivyo, anakubali kuwa si
rahisi kuishi katika jiji kubwa. Kwa nini? Kwa
sababu watu huathiriwa sana wanapoishi
miongoni mwa watu wenye tamaa ya mali.
Anasema hivi: “Huku jijini, mali huonwa kuwa
muhimu sana.” Kwa wazi, uvutano wa marika si
mchezo. Basi, ni kwa nini vijana wengi hufikiri
kwamba hawawezi kuathiriwa na marika wao?
Kuathiriwa Sana Bila Kutambua
Marika wanaweza kumwathiri mtu bila yeye
kujua. Kwa mfano: Tunapokuwa kwenye usawa
wa bahari, hewa iliyo juu yetu huendelea
kutushinikiza. Kila sehemu yenye ukubwa wa
sentimeta moja ya mraba hupata shinikizo la
kilogramu moja. * Huenda unashinikizwa hivyo
kila siku bila kujua. Kwa nini? Umezoea.
Ni kweli kwamba shinikizo la hewa haliwezi
kudhuru. Lakini watu wanapotushinikiza bila sisi
kujua, wanaweza kutufanya tubadilike pole kwa
pole. Mtume Paulo alijua kwamba watu
wanaweza kuathiriwa sana na wenzao.
Aliwaonya hivi Wakristo huko Roma: “Msiache
ulimwengu unaowazunguka uwafinyange
kulingana na muundo wake.” ( Waroma 12:2 , The
New Testament in Modern English) Tunaweza
kujipataje katika hali hiyo?
Jinsi Watu Wanavyoathiriwa na Marika
Je, wewe hupenda kukubaliwa na wengine?
Wengi wetu wanaweza kukubali jambo hilo. Hata
hivyo, tamaa yetu ya asili ya kukubaliwa inaweza
kuleta faida au madhara. Je, sisi hufanya juu
chini ili tukubaliwe na wengine? Hata ikiwa tuna
uhakika kwamba hatuwezi kuathiriwa na marika
kiasi hicho, vipi watu wengine tunaoshirikiana
nao? Je, wanajaribu kuepuka kuathiriwa na
marika wao, au wanajiachilia wafinyangwe nao?
Kwa mfano, watu wengi leo huona kwamba
viwango vya Biblia kuhusu maadili ni vya
kizamani ama havifai katika ulimwengu wa sasa.
Wengi wanaonelea kwamba si lazima kumwabudu
Mungu kulingana na matakwa yake yaliyo katika
Neno lake. ( Yohana 4:24 ) Kwa nini wanaonelea
hivyo? Huenda sababu kuu ni kwamba
wameathiriwa na watu wengine. Kwenye
Waefeso 2:2 , Paulo anasema kwamba kuna
“roho” fulani au mtazamo fulani ulioenea katika
mfumo wa mambo. Roho hiyo huwachochea
watu wafikiri k**a watu wa ulimwengu
wasiomjua Yehova. Tunaweza kuathiriwaje?
Shughuli tunazofanya kila siku, k**a vile kwenda
shuleni, kujifunza, kutunza madaraka ya familia,
na kufanya kazi hutulazimu tushirikiane na watu
ambao hawafuati maadili ya Kikristo kikamili.
Kwa mfano, huenda shuleni kuna vijana wengi
ambao wanajitahidi kwa udi na uvumba kuwa
mashuhuri, wanaofanya uasherati, au hata
wanaotumia dawa za kulevya na pombe. Ni nini
kinachoweza kutukia tukiwa na marafiki
wanaofanya mambo hayo au wanaoyaona kuwa
ya kawaida, au hata kuwa mazuri? Huenda
tukaanza—pole kwa pole—kuiga mwenendo wao.
“Roho,” au “hewa,” ya ulimwengu itatuathiri sana
na kutufanya tuwe k**a watu wa ulimwengu.
Wataalamu wa mambo ya kijamii wamefanya
majaribio fulani ambayo yanaunga mkono kanuni
hizo za Biblia. Hebu fikiria lile jaribio maarufu la
Asch. Katika jaribio hilo, mtu huombwa ajiunge
na kikundi cha watu walioketi pamoja. Dakt.
Asch huwaonyesha watu hao kadi kubwa yenye
mstari ulio wima, kisha anawaonyesha kadi
nyingine yenye mistari mitatu iliyo wima yenye
urefu mbalimbali. Halafu anawaomba watu walio
katika kikundi hicho wachague mstari
unaofanana na ule mstari wa kwanza. Jibu ni
rahisi. Mara chache za kwanza, wote
wanakubaliana. Lakini wanapoulizwa swali
hilohilo mara ya tatu, mambo yanabadilika.
K**a ilivyokuwa mara zile nyingine, ni rahisi
kuchagua mistari inayofanana. Lakini yule mtu
anayejaribiwa hajui kwamba washiriki wale
wengine wa kikundi hicho wamelipwa ili kufanya
jaribio hilo. Sasa, wanapoulizwa swali hilo mara
ya mwisho wote katika kikundi wanaamua
kuchagua mstari usiofaa. Matokeo huwa nini? Ni
asilimia 25 tu ya watu wanaojaribiwa hivyo
ambao huchagua mstari sahihi kwenye jaribio
hilo la mwisho. Lakini wengine wote hufuata
maoni ya kikundi angalau mara moja—hata
ingawa wao wenyewe wanaona kwamba mistari
hiyo hailingani!
Ni wazi kwamba watu hutaka sana kukubaliwa na
watu wanaoshirikiana nao hivi kwamba
wanaweza kukataa mambo wanayojua kuwa ya
kweli. Vijana wengi wameathiriwa hivyo. Daniel,
mwenye umri wa miaka 16, anakubali hivi:
“Vijana wenzako wanaweza kukufanya ubadilike.
Na unapokuwa kati ya watu wengi, uvutano huo
huongezeka. Unaweza hata kuanza kufikiri
kwamba wanafanya mambo mazuri.”
Angie, aliyenukuliwa hapo awali, anaeleza jambo
lililotukia shuleni: “Nilipoingia katika shule ya
sekondari, hungevalia nguo zozote tu. Vijana
walipenda kuvalia nguo zenye lebo. Iliwabidi
vijana wanunue shati za dola 50 za Marekani
wapende wasipende.” K**a vile Angie
anavyosema, ni vigumu kujua kwamba
unaathiriwa na vijana wengine. Lakini je,
tunaweza kuathiriwa na vijana wenzetu kufanya
mambo mabaya hata zaidi?
Hatari za Kuathiriwa na Marika
Hebu wazia ukiogelea baharini. Unapozidi
kuogelea na kupelekwa na mawimbi, huenda
kukawa na nguvu nyingine ambazo huzitambui.
Mawimbi hayo yanakusukuma kuelekea ufuoni,
lakini huenda kuna mkondo mwingine chini ya
maji. Pole kwa pole mkondo huo unakusukuma
huku na huku. Kufumba na kufumbua, huwaoni
tena watu wa familia yako au marafiki wako
unapotazama ufuoni. Kumbe hukutambua
kwamba mkondo wa maji ulikusukuma mbali
sana! Vivyo hivyo, tunapoendesha shughuli zetu
za kila siku, mawazo na hisia zetu huathiriwa
daima. Pasipo kujua, tunaweza kuathiriwa
tupuuze kanuni ambazo tulifikiri tungezishikilia
kwa uthabiti.
Kwa mfano, mtume Petro alikuwa mwanamume
jasiri. Usiku ule ambao Yesu alik**atwa, Petro
alitumia upanga mbele ya umati wenye hasira
kali. ( Marko 14:43-47; Yohana 18:10 ) Hata hivyo,
miaka mingi baadaye aliathiriwa na watu na
akaonyesha ubaguzi wa wazi. Aliwahepa
Wakristo Wasio Wayahudi—hata ingawa hapo
awali Kristo alikuwa amemwonyesha njozi
ambayo ilimwongoza asiwaone Wasio Wayahudi
kuwa wasio safi. ( Matendo 10:10-15, 28, 29 )
Huenda Petro alihisi vigumu zaidi kudharauliwa
na watu kuliko kukabiliana na watu wenye
mapanga! ( Wagalatia 2:11, 12 ) Pasina shaka,
uvutano wa marika unaweza kuwa hatari.
Ni Muhimu Kujua Kwamba Marika Wako
Wanaweza Kukuathiri Sana
Mfano wa Petro unaweza kutufundisha somo
muhimu. Kuwa na sifa fulani nzuri hakumaanishi
kwamba mtu hana udhaifu wowote. Petro alikuwa
na udhaifu, k**a sisi sote. Haidhuru sisi ni nani,
tunapaswa kufahamu udhaifu wetu. Tunaweza
kujiuliza hivi kwa unyoofu: ‘Udhaifu wangu ni
nini? Je, mimi hutamani utajiri? Je, nimeanza
kujivuna kwa sababu ya sura yangu au mafanikio
yangu? Je, ninaweza kufanya lolote liwalo ili
nipate sifa, cheo, na umashuhuri?’
Naam, huenda tusijiletee balaa kimakusudi kwa
kushirikiana na watu wanaotumia dawa za
kulevya au wanaofanya uasherati. Lakini vipi
kuhusu udhaifu wetu mbalimbali uliofichika?
Tukichagua kushirikiana kwa ukaribu na watu
ambao wanafanya mambo mabaya
yanayohusiana na udhaifu wetu, basi tutakuwa
tunajiachilia tuathiriwe nao—na labda tunaweza
kuangamia kabisa.
Hata hivyo, inatia moyo kukumbuka kwamba kuna
uvutano unaofaa. Je, tunaweza kutumia uvutano
huo vizuri—kwa faida yetu? Na tunawezaje
kuepuka kuathiriwa vibaya na marika? Maswali
hayo yatajibiwa katika makala moja ya wakati
ujao ya “Vijana Huuliza . . . ”

Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Careen minde posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share