27/11/2022
Hadith:Firimbi.
Mtunzi:Ladislaus Mude.
Sehemu:-8
Makiwa alipofikisha umri wa miaka kumi na moja na wakati huo Mama yake alikuwa tayari ameshafariki, Makiwa alibaki mkiwa hakuwa na furaha tena ya kuishi alitamani kujiua ili apishane na fedhea na manyanyaso ya vijana wenzake.
Akiwa ndani ya usingizi mzito Makiwa atokewa na kitu cha ajabu ajabu upepo si upepo kimbunga si kimbunga kitu hicho cha ajabu kiliongea na Makiwa na kumwambia Makiwa mwana mnyonge wa Chimve, mkombezi na shujaa wa kweli yanini kukata tamaa?, tumekuleta wewe, tumekuchagua wewe ili uiokoe Chimve na watu wake wewe ni uzao wetu ”
Makiwa aduwaaa na kushikwa na uoga moyoni upepo wa ajabu waendelea kusema”usifadhaike moyoni mwako, faraja yako ipo Chimve, itumie vizuri ili ikupe furaha, Aonyeshwa Njiwa akiwa amelalia yai ndani ya pango katikati ya misitu mkubwa na juu ya kilele cha jabari kubwa nje kidogo ya mji wa Chimve.
Makiwa aamshwa usingizini ikiwa ni usiku wa Manani na kuelekea kule alipo onyeshwa na Mizimu, palikuwa ni usiku mkubwa lakini cha ajabu eneo lile palikuwa na mwanga wa ajabu mithili ya theruji ya mlima ulipo nyikani mwa mashariki ya bara giza.
Hakika huwezi kuungalia kwa macho meupe aingia moja kwa moja mpaka pangoni akielekezwa na kipofu jongooo amkuta njiwa mweupee peee akiwa anatamia yai, hakika mbwa hulala chali akimuona bwana wakenjiwa alipo muona Makiwa anaingia alisogea pembeni na kuliacha yai pekeyake.
Makiwa achukua yai lile kitendo cha kulishika tu yai likabadilika na kuwa Firimbi inayo ngaaa, mngao wa dhahabu Makiwa ashtuka toka usingizini na kujikuta akiwa katika msonge wake wa suti mkononi akishika firimbi ya yake.
Firimbi ilikuwa na maajabu mengi kwanza hupigwa na mtu mmoja pili hupigwa kwa kutumia tundu za pua wakati wa shida maalum au panapo hitajika msaada wa jambo fulani sio mdomo, kipindi inatoa sauti basi maadui wote upatwa na usingizi mzito pia hutoa sauti inayo burudisha, kuliwaza na kukupa tumaini, firimbi hiyo ya ajabu huja kipindi cha tukio tu na hubadirika kutokana na matukio na sehemu.
Makiwa aingiwa na uoga na hakuamini alichonacho mkononi kwani alijua ni ndoto tu aliamua kuendelea na utamaduni wake wa kuimba na kupiga firimbi, watu wengi walimdharau na kumuona ni mtu fukara na ombaomba vijana wenzake walimtenga kisa alizaliwa na wazee na wengine kumuita mtoto wa ajuza wengine kumuita mtoto wa mkorechi.
Mizimu ya Chimve ilimpenda Makiwa kwani ndio lililozao lao la pekee nje ya ukoo wa Chifu na walimlinda kwa kila janga walifanya kila liwezekanalo Makiwa aishi ingawa hawakuweza kumpata akili ya utambuzi juu ya matumizi ya firimbi yake ya ajabu.
UGENI WA MGENI.
Siku zimepita mgeni azoea Chimve watu walizidi kumshangaa mgeni washindwa elewa nani kaja nini kafata, mgeni alikuwa ni mtu tofauti na watu wa Chimve kitabia na kimuonekano watu wengi walihisi ni miujiza ya Mizimu kuleta kiumbe kile ingawa kilikuwa kinaongea na kuandika.
Rangi ya mwili wake nik**a tunda la mpapai, mwili wake una vinyweleo k**a ngozi ya kondoo nywele zake laini k**a nyuzi za fusi macho makali yenye kumetameta k**a vito vya kuta wa mji wa Chimve, hekima yake ipo juu mithili ya ndege njiwa, kinywa chake kitamu k**a ndege kasuku sura yake ya upole k**a nyani mtegoni hakika wana Chimve walistaajabu kumuona kiumbe kile.
Kutokana na utofauti wake Wana-Chimve walimpeleka mpaka kwa Chifu wao Chemvue, Chemvue alimkaribisha na kumpa kibuyu cha ugimbi k**a ishara ya ukaribisho na kumfanya awe huru na Amani Chemvue alimuhoji yeye ni nani amekuja kufanya nini.ingawa lugha iliyotumika ni ishara na michoro tu.
Itaendelea............