02/01/2019
James & Jennifer - Familia ya Siku Tano
Kupata mwendelezo wa hadithi hii/kitabu chote tafadhali wasiliana nami kwa WhatsApp 0764688786.
SURA YA KWANZA - JUMANNE.
Ilikuwa majira ya mchana jijini Dar es Salaam. Joto lilikuwa kali, kila anaetembea mkononi ameshika kitambaa akifuta jasho, au gazeti akijipepea. Gari dogo aina ya Toyota IST jeusi lilisimama, kisha mwanamume wa makamo alishuka pole pole. Mkononi alishika mkufu mdogo akiuchezea chezea. Macho yake yaliitazama shule ya msingi iliyo mbali kidogo.
Adam aliitazama saa yake ya mkononi, kisha akainua macho kuitazama shule. Alijifuta jasho kwa kiganja, kisha akarudi ndani ya gari. Hapana chezea joto la Dar, k**a una AC lazima uifuate. Akiwa ndani ya gari, Adam anainama, anatoa picha ndogo kwenye wallet yake na kuitazama. Picha hii ni ya mwanamke mrembo, aitwaye DIANA. Adam aliitazama picha kwa muda, akiwa na mawazo kichwani, huku anapitisha vidole vya mkono wa kulia taratibu akiipapasa.
Kisha alitoa picha nyingine ndogo. Hii ilikuwa ni ya watoto wawili mapacha wa kiume na k**e. Anaitazama kwa muda. Anazishika kila moja na mkono wake na kuzitazama kwa zamu k**a anazifananisha. Anatazama picha ya watoto na kuinua macho kutazama shule.
Adam anarudisha picha. Anatoa mkufu na kuutazama tena anainua macho kuitazama shule. Wanafunzi wanatawanyika kwa mbali.
Kundi kubwa la wanafunzi walikuwa wakikimbia kutoka upande wa shule, ilionekana ni muda wa kurudi nyumbani. Wanafunzi wawili wa k**e (JENNIFER) na kiume (JAMES) walikitembea kutokea shuleni.
Jenifer alitembea akicheza na kuruka ruka. Kisha, alikimbia mbele ya kaka yake. Anageuka kurudi kinyumenyume akicheza singeli. James aliishia kutingisha kichwa akicheka tu.
Adam anawasha gari na kuwafuata James na Jennifer polepole. Anawakuta mbali kidogo na shule. Anasimamisha gari pembeni yao. Jennifer na James wanasimama. Kioo cha gari kinashushwa na sura ya Adam inaonekana.
JENNIFER
Shikamoo we mbaba
ADAM
Marahaba, za shule?
JENNIFER
Nzu…….
James anamshika mkono Jennifer na kumvuta kuanza kuondoka. Adam anasogeza gari polepole na kusimama tena mbele yao.
ADAM
Hebu simameni, nyi ni James na Jennifer Mahinya?
JAMES
Ndio ni sisi, we nan na unataka nini?
ADAM
Mi ni afisa wa polisi,mama yenu ameniagiza. Ingieni niwapeleke alipo.
Adam anatoa pochi yake na kuifungua akiwaonyesha kitambulisho.
JAMES
Amekutuma mama?
ADAM
Ndio, amese…..
JAMES
Amesemaje? Kwani akutume wewe? mwenye yuko wa?
ADAM
Kuna ajali ndogo imetokea, mama yenu hajaumia ila amepumzishwa
Muhimbili.
JENNIFER
Anaendeleaje? imekuwaje?
ADAM
“Kuna moto ulitokea saloon kwake, hajaungua ila moshi ulimfanya azimie kwa muda, kaniomba niwapeleke Muhimbili.”
Jennifer anasogea karibu na gari. Anashika mlango wa gari kutaka kuingia. James anamshika mkono na kumvuta nyuma yake.
JAMES
Ngoja Jenny, k**a we polisi mbona hujavaa nguo za kipolisi?
ADAM
Kwenye kikosi chetu hatuvai sare, umeshawah kuskia askari kanzu?
JAMES
Ndio nawajua, mi sikuamini, nimeskia watu wanaiba watoto wanatengezea mafuta ya ndege.
Adam anatabasamu, kisha anacheka
ADAM
Hapana James, haiwezekani kutumia mwili wa mtu kutengeneza mafuta ya
ndege, mafuta ya ndege yapo ya aina tatu Jet A, Jet A 1 na Jet B,
yanatengenezwa kwa kuchanganywa, Hydrocarbons mbalimbali zenye
molecular weight tofauti tofauti, sawa eh?
JENNIFER
Unatumia maneno magumu magumu tusielewe enh? kwanza kwan we rubani?
ADAM
Si nimewaambia mi ni afisa wa polisi? mbona mnakuwa na maswali
mengi mengi? ingieni garini twende, au nikamwambie mmekataa?
JAMES
Hapana, tunataka uhakika kuwa kweli amekutuma, mpigie simu tuongeee nae.
ADAM
Unategemea saloon yake imeungua, ye…ametoka kazimia atakuwa amekumbuka
simu?….huh?
JAMES
Mhhhh sawa ila alituambia akimtuma mtu atamtajia jina maaalumu, we
kakwambia jina gani?
ADAM
Kasema nije kuwafata kunguru wake wa Zanzibar
JENNIFER
Hapo sawa, twende James kweli mama kamtuma.
Jennifer anafungua mlango wa nyuma na kuingia, James anafata polepole pole nyuma yake na kuingia. Adam anawasha gari na kuondoka taratibu. Gari inasimama nje ya duka kubwa la vyakula. Adam anageuka kuwatazama James na Jennifer waliokaa viti vya nyuma.
ADAM
Shukeni niwanunulie chochote cha kula, najua mtakuwa na njaa.
JENNIFER
Utamdai mama hela au huruma zako tu we mbaba? Mr…
Jennifer anainua mkono akimtazama Adamu na kupiga saluti anapozungumza.
JENNIFER (CONT’D)
Mr…Mr…Policeman
ADAM
ADAM, naitwa Mr ADAM MOSHA aya twendeni.
Wanashuka wote watatu na kuelekea kwenye mgahawa. Wanakaa na muhudumu anasogea.
ADAM
Tupe chipsi kuku kwa ajili ya Jennifer hapa na ubwabwa maini kwa ajili ya James.
JENNIFER
We mbaba mchawi nini, umejuaje hivo ndo vyakula tunavovipenda? James tumkimbie huyuuu, tumekutana na shetani.
Jennifer anasema akimtazama Adam na James kwa zamu. Kisha ananyanyua mikono na kutengeneza makucha kwa vidole vyake k**a paka akimtishia James anapotamka shetani. Adam anacheka kwa nguvu, anamtazama Jennifer kwa mapenzi makubwa.
ADAM
You are so funny Jennifer, umesahau mimi ni polisi? Tena polisi mpelelezi, tukiwa
chuoni tunafundishwa Psychology, jinsi ya kumsoma mtu bila hata
kumuuliza chochote, kwa mfano hapa nimekutazama machoni nimejua unapenda nini.
Jennifer anashika shavu lake na kufikiria kidogo, kisha anainua uso.
JENNIFER
Mhhh k**a kweli niambie, mi napenda rangi gan?
ADAM
Mhhh ngoja niwaze kidogo…. Okey umebeba beg la pink, niliona kalamu
yako ya pink pia ndani ya gari, ulipokuwa unaingia garini niliona
pia umevaa tight ya pink, naamini hata uniform mngekuwa mnaruhusiwa
ungevaa ya pink pia, so rangi uipendayo ni pink, uwongo uwongo?
JENNIFER
Duh we mkali unachungulia hadi watoto
Wote wanacheka, Adam anaonekana kuwa na furaha zaidi. Muhudumu anawaletea chakula.
MUHUDUMU
Samahani kaka, we hukuangiza chochote?
ADAM
Oh usijali, niletee Juice na Sambusa k**a mnazo
Muhudumu anaondoka, Jennifer anainua uma na kumuelekezea Adam.
JENNIFER
Usiwe unapenda kula sambusa we mbaba polisi umeskia eh?
ADAM
Kwanini mwanangu? mbona nzuri tu?
Jennifer anainua mkono na kuuweka k**a anataka kumnong’oneza Adam. Adam anasogeza kichwa.
JENNIFER
Ujue siku izi kuna mgao wa umeme kwa hiyo mashine za kusagia nyama hazifanyi kazi,
ADAM
Mh sijajua hilo linahusiana vipi na kusema nisile sambusa.
JENNIFER
Mapolisi wa siku izi bwana, wanataka kufundishwa kila kitu yan
Adam anacheka. Anatoa notebook na peni kwenye mfuko wa shati na kujifanya anaandika anachosema Jennifer.
ADAM
Ujue ukimdhalilisha polisi nina haki ya kukuk**ata? Lakini kwa kuwa
kweli sijui aya nakusikiliza mwalimu, nimeshakaa tayari na kuandika ufundishacho.
JENNIFER
Ni hivi, k**a mashine hazifanyi kazi manake wanashindwa kusaga
nyama kwa hiyo wanakodi watoto wawe wanatafuna nyama ila hawamezi
wanatemea kwenye beseni had zijae ndo wanaenda kutengenezea sambusa.
Adam anacheka sana, muhudumu aliekuwa kasimama nyuma ya Jennifer akimsikiliza anacheka pia. Jennifer anageuka anashtuka anapomwona na kuziba mdomo wake kwa mkono. Muhudumu anaweka Juice na sambusa za Adam mezani na kumpiga Jennifer na tissue papers alizokuwa nazo mkononi. Kisha anageuka na kuondoka.
Wanaendelea kula taratibu. Wanamaliza na kurudi garini. Wanaingia na safari inaanza tena.
ADAM
Okey, so watoto wazuri, mna mpango wa kuwa nani mkiwa wakumbwa? Jenny?
JENNIFER
Mh nina mpango wa kuwa Jenny mkubwa
ADAM
Hahahah aya umeshinda, una mpango wa kufanya kazi gani?
JENNIFER
Wakili
ADAM
Mwanasheria? kwanini?
JENNIFER
Ujue siku unapopata leseni ya uanasheria unapata na leseni ya
kudanganya.
Adam anacheka, anageuka nyuma na kurudisha macho barabarani.
ADAM
Mhhhh ila we unawezaje kujua wakili anadanganya?
JENNIFER
Mbona rahisi tu, ukitaka kujua wakili anadanganya angalia utaona
mawakili wenzake wanavutiwa na anachosema, au unamsikiza tu kwa
saabu vyote anavosema ni uongo tu
ADAM
Hahahahah haya Jenny! na James je? unataka kufanya nini ukubwani?
James anaonyesha kuboreka, anatazama nje na kuona mabango yanaonyesha wanaelekea Morogoro, anashtuka na kuangalia nyuma. Anainama mbele.
JAMES
We mbaba, hi sio njia ya Muhimbili, hii njia ya Kibaha, turudishe kwa
mama, unatupeleka wapi??
ADAM
Tunaelekea nyubani kwangu
JENNIFER & JAMES
Wapi????????
ADAM
Nyumbani kwangu
James na Jennifer wanatazamana. Kisha wanakumbatiana. Jennifer anaficha uso kifuani kwa kaka yake.
USIKU: SEBULENI KWA DIANA
Diana amekaa kwenye kochi. Anasimama na kuzunguka zunguka sebuleni. Anashika simu na kuiweka mezani tena. Anainua macho kutazama saa ya ukutani. Inaonesha ni saa mbili na nusu usiku. Simu ya mezani inaita. Anakimbia haraka na kuinyanyua
DIANA
Hallo!..hallo!…hallo!
Amesimama na simu ukutani hasikii chochote
DIANA
Hallo, we nan? k**a huna watu wa kuongea nao, piga simu redion
uongee na watangazaji, we mlinzi huna wa kuku kampani nini?
Diana anainua mkono mwingine usio na simu na kuikata. Kisha anarudisha mkono wa simu na kugeuka. Simu inaita tena. Anainyanyua kwa hasira.
Adam amekaa ndani ya gari ikiwa na mwanga mdogo. Ameshika simu kwa mkono wa kushoto ikiwa sikioni. Mkono wa kulia ameshika picha ya Diana akiitazama sana.
DIANA
We nani usie na kazi ya kufa…..
ADAM
Diana, mi ni Adam!
DIANA
Adam, Adam yup, yule alieshawishiwa na Eva au? unataka nini kwangu?
ADAM
Diana, ninao watoto!
DIANA
Whaaat? We unanjua unanskia?
ADAM
Diana, ninao watoto, ninao watoto wetu!
DIANA
Hiv we mzima kweli, una watoto na nan? Nataka wanangu kabla sijaita
polisi, we nan lakini?
ADAM
Mimi ni Adam, umenisahau? Lazima ulijua nitarudi.
DIANA
Nimesahau? Sijakusahau ila sikujui kabisa, and this is not funny, got it?
ADAM
Baba wa watoto, baba wa kweli wa Jenniffer na James. Diana anatoa macho, anapooza gafla anatereza ukutani pole pole na kukaa chini, simu akiwa kaishikilia begani.
ADAM
Diana, are you okay, nijibu please.
Diana analia taratibu, hajibu kitu mkono mwingine amejishika kichwani, machozi yanamdondoka
ADAM (CONT’D)
Diana, mbona hujibu? Kumbuka ninao watoto, naweza kuwafanya chochote
k**a tusipoelewana.
DIANA
Kwa nini lakin, kwa nini unanifanyia hivi? uliyoisha fanya hayatoshi?
ADAM
Nakupenda Diana, daima nimekupenda, nawapenda na wanetu pia,
nataka kuitunza familia yangu
DIANA
Jaman please, warudishe wanangu, nakuomba nipo chini ya miguu yako.
Adam ameshika simu, hajibu kitu, anaonyesha huzuni. Diana anasimama na kutembea tembea sebuleni. Anapaza sauti
DIANA
Nataka wanangu, unaskia we mbakaji, nataka wanangu nasema ntakufanyia
kitu mbaya wewe ohoooo.
ADAM
Diana! kunifokea hakusaidii, wapo salama nyumbani kwangu,
wapo nyumbani kwetu, kwako na kwangu.
DIANA
Unataka nin kwangu lakini?
ADAM
Nataka uje, uje tutengeneze familia pamoja, kumbuka ukitoa taarifa polisi au
kwa mtu mwingine yoyote, hutawaona watoto tena, nakupenda
sana Diana,
DIANA
Upo wap niwafate?
ADAM
Hapana! siwezi kukuambia kwa sasa.
DIANA
Adam, watoto wako wapi nataka kuongea nao, mpo wapi niwafate?
ADAM
Hapana haiwezekan! muda huu bado wamelala nyumbani.
DIANA
Umewaacha na nani, wako peke yao? Nataka kuona wanangu jamani!
ADAM
Haswaa utawaona usijali! na ndio sababu nimekupigia, kwanza hakuna
litakalo kuwa sawa bila uwepo wako.
DIANA
Itabidi nijue mpo wapi
ADAM
Ntajuaje k**a hutawaambia watu wengine? Au kuja na polisi kabisa?
DIANA
Adam, siwezi kufanya hivyo, k**a polisi ningeshatoa taarifa tayari! siwez kufanya hivyo, ntahatarisha, maisha ya wanangu, nipo tayari kwa lolote kupata wanangu.
Adam ameegemea gari. Anatembea taratibu na kurudi kuegemea gari. Mazingira na porini na kweusi sana. Hajibu kitu kwa muda.
DIANA
Jaman, please mbona hutaki kunielewa?
ADAM
Diana, nasikitika we ndo hutaki kunielewa, nataka uwe ni uamuzi wako
sio wangu. Sitajaribu kukulazimisha kuja, nipo tayari kukusubiri hata maika ishirini,
ila siku ukija inakuwa moja kwa moja. I want this to be right.
DIANA
Ila nataka kuja, nataka kuwa na wewe, nataka kuwa na familia yangu yote.
ADAM
Unamaanisha lakini Diana? huwa Sina masihara kwenye uwongo.
DIANA
Sijawah kuwa serious k**a leo maishani mwangu.
ADAM
Sawa k**a ni hivyo, sa ivi ulale kwa amani, watoto wapo salama, ntakupigia simu
sa moja asubuhi kukuelekeza, kumbuka, No police and everything will be okay, I love you
DIANA
Nataka kuongea nao….. hallo! ngoja usikate si… hallo! hallo!
Kupata mwendelezo wa hadithi hii/kitabu chote tafadhali wasiliana nami kwa WhatsApp 0764688786.