TAFCA Shirikisho

TAFCA Shirikisho Ukurasa rasmi wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania - TAFCA

06/07/2026

Kodi lukuki zinavyowaumiza wasanii wachongaji wa Tanzania.

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo (MICAS)
Ukurasa Rasmi wa Wizara ya Utalii - Tanzania🇹🇿
Ikulu Tanzania
Baraza la Sanaa (BASATA)

03/07/2026

Sekta ya utalii na sanaa nchini inatarajiwa kupata msukumo mpya kupitia Tamasha la Sanaa na Kazi za Ufundi litakalofanyika mwezi Oktoba mwaka huu, likiwa na dhamira ya kuhamasisha uchumi wa ubunifu, kutangaza utamaduni wa Tanzania na kuwafungulia wasanii masoko ya ndani na kimataifa.

Tamasha hilo linaandaliwa na Tanzania International Tourism Festival (TITF) kwa kushirikiana na Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA), likiwakutanisha wachongaji, wachoraji, wabunifu wa mavazi, watengenezaji wa vito, wafinyanzi na wasanii wengine wa kazi za mikono kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Grand Melia Arusha, Mkurugenzi wa Tanzania International Tourism Festival, Ibrahim Jamal, amesema tamasha hilo limebeba maono ya kuiunganisha sekta ya sanaa na utalii ili kuongeza thamani ya kazi za ubunifu na kuwapa wasanii fursa za kibiashara.

Amesema mbali na maonesho ya sanaa, washiriki watapatiwa mafunzo kuhusu uongezaji thamani wa bidhaa, ulinzi wa haki za kazi za ubunifu, pamoja na mbinu za kufikia masoko ya ndani na nje ya Tanzania kupitia sekta ya utalii.

27/06/2026
BURIANI MOSES LUHANGATasnia ya Sanaa za Ufundi hususan Fani ya uchoraji nchini Tanzania imepata pigo kwa kumpoteza mchor...
26/06/2026

BURIANI MOSES LUHANGA

Tasnia ya Sanaa za Ufundi hususan Fani ya uchoraji nchini Tanzania imepata pigo kwa kumpoteza mchoraji mashuhuri Moses Luhanga ambaye amefariki dunia jioni ya leo jijini Dar es salaam. Luhanga ni miongoni mwa wachoraji wa sanaa za uchoraji (visual artists) waliojijengea jina nchini Tanzania na Afrika Mashariki kupitia maonesho ya ndani na ya kimataifa.

Ni msanii wa uchoraji aliyefanya kazi kwa miaka mingi nchini Tanzania, hasa akiwa Dar es Salaam.
Luhanga amehusika katika maonesho mbalimbali ya sanaa yanayolenga kuitangaza sanaa ya Tanzania ndani na nje ya nchi.

Kazi zake zinajulikana kwa kuonyesha mandhari za asili, wanyamapori, na uhalisia wa maisha ya kila siku ya mtanzania.

Baadhi ya maonesho aliyoshiriki Moses Luhanga ni Mradi wa "14 Voices" mwaka 2017, uliowakutanisha wasanii 14 wa Tanzania kwenye maonesho nchini Kenya kwa lengo la kutangaza sanaa ya Tanzania na kujenga ushirikiano wa kikanda.

Alishiriki pia kwenye kampeni ya "Dawati ni Elimu", ambapo wasanii walichora kazi za sanaa kwa ajili ya kuchangisha fedha za kuboresha mazingira ya elimu nchini.

Marehemu Luhanga pia alishiriki maonesho katika kituo cha sanaa cha Kuona Trust nchini Kenya, ambapo kazi zake zilioneshwa pamoja na za wasanii wengine mashuhuri wa Tanzania.
Mtindo wake wa uchoraji unahusishwa zaidi na:
- Uhalisia (realism)
- Michoro ya wanyamapori
- Mandhari za Afrika
- Matumizi ya rangi zenye mvuto na maelezo ya kina katika uchoraji.

Msiba uko nyumbani kwa marehemu Kinondoni Hananasif, Dar es Salaam.

Rais wa TAFCA Bi Rukia Walele anatoa pole kwa familia ya marehemu na anaungana na wanasanaa hususani wachoraji wote nchini katika kuomboleza kifo cha Moses Luhanga.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, AMEN.

Rais wa TAFCA Bi. Rukia Walele leo ameungana na viongozi mbalimbali, wasanii na wananchi kushiriki kwenye msiba na mazis...
13/06/2026

Rais wa TAFCA Bi. Rukia Walele leo ameungana na viongozi mbalimbali, wasanii na wananchi kushiriki kwenye msiba na mazishi ya Mzee Onyango, msanii nguli wa maigizo na filamu aliyefariki juzi na kuzikwa leo jijini Dar e salaam.
TAFCA inatoa pole kwa tasnia ya filamu kwa kumpoteza msanii huyu aliyejizolea umaarufu mkubwa kwa aina yake ya uigizaji tangu enzi za michezo ya redioni kupitia Radio Tanzania na baadae kwenye tamthilia na filamu mbalimbali.

Rais wa Shirikisho la sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA) Bi Rukia Auliae Walele akiwa na rais wa Shirikisho la Sanaa za Ma...
13/06/2026

Rais wa Shirikisho la sanaa za Ufundi Tanzania (TAFCA) Bi Rukia Auliae Walele akiwa na rais wa Shirikisho la Sanaa za Maonesho (SHISAMA) Dr. Cynthia Henjewele wamewawakilisha wasanii wa makundi mbali ya sanaa nchini kwenye hafla ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania. Hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan imefanyika katika Ukumbi wa JINCC, Jijini Dar es Salaam.

Shisama_Tanzania
Rukia Walele #
Dkt. Cynthia Mwambeleko Henjewele

14/04/2026

Hafla ya Ugawaji wa Mirabaha na Utoaji Mikopo kwa Watengeneza Maudhui mitandaoni, tarehe 18 April, 2026.



Katibu Mkuu wa TAFCA Bw. Marco Tibasima (kulia) hii leo amehudhiria ufunguzi wa Kikaokazi cha 16 cha Maafisa Utamaduni n...
28/03/2026

Katibu Mkuu wa TAFCA Bw. Marco Tibasima (kulia) hii leo amehudhiria ufunguzi wa Kikaokazi cha 16 cha Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya Michezo nchini. Kikao kazi hicho cha siku 4 kilichofunguliwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Christian Makonda (Mb) kinafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa AICC jijini Arusha. Mhe. Makonda amemwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Mwigulu Nchemba. Katikati ni Mwenyekiti wa Chama cha Waigizaji Tanzania Bw. Chiki Mchoma, kushoto ni Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Bw. Rajab Ameir.

Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when TAFCA Shirikisho posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to TAFCA Shirikisho:

Shortcuts

Share