11/11/2025
MAISHA NI MAOMBI
"Hata Uonekane Umekauka na Kufa, Usiogope, Utachipua Tena"
Ayubu 14:7 "Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena, Wala machipukizi yake hayatakoma."
Katika Maisha haya, kuna wakati Mtu anaweza kupitia wakati mgumu hadi anahisi hakuna maisha tena. Hali yake inakuwa haina tofauti na mti uliokauka katika hali ya kiangazi Jangwani.
Inawezekana mtu mmoja hapa anapitia hali ngumu ambayo haoni tumaini mbele, huenda ni ugonjwa, Inawezekana ni madeni, Inawezekana ni mahusiano, Inawezekana ni ndoa, Inawezekana ni mambo ya familia, Inawezekana ni nguvu za giza, Inawezekana ni maisha magumu, Je ni jambo gani gumu unalipitia?
Usihofu, endelea kumtazama Mungu kwa Imani, bado kuna maji ya uzima kutoka kwa Yesu, zidi kumtumaini yeye, nawe Utachipua na Kustawi Tena. Kwa Mungu yote yanawezekana.
NAKUTAKIA SIKU NJEMA YENYE KUJAA BARAKA ZA BWANA NA MATUMAINI.