03/11/2022
JE, WAJUA?๐ค
Mwaka jana mwishoni, tetesi za Umoja wa nchi za Ulaya kuweka sheria ya simu zote kuwa na port ya USB-C ili kuweka umoja wa cable na kupunguza takataka za kielektroniki: Apple ilikuwa ni kampuni ambayo ilipata changamoto kwa sababu haitumii port ya USB-C katika simu zake za iPhone.
Kampuni nyingi hasa za simu za Android mfano Infinix, Samsung, Google, Nokia, Motorola, Oppo, Vivo, n.k tayari zimehamia kwenye port ya USB-C.
Tetesi za mwanzo zilionyesha Apple italazimika kuweka port ya USB-C katika iPhone. Na tayari Apple ilikuwa imeanza majaribio ya kiufundi katika iPhone 13 na iPhone 14.
Jana uthibitisho umetoka rasmi ndani ya kampuni ya Apple. Mtendaji mkuu wa Apple - Greg Joswiak na Craig Federighi ambaye ni Makamu wa Rais mkuu wa Masoko wamethibitisha katika Interview ya Wall Street Journal kuwa Apple inaweka USB-C kwenye iPhone ili kuendana na kanuni mpya za EU.
Inaonekana iPhone 15 ndio itakuwa iPhone ya kwanza kuwa na USB-C!
Credits: .tek