Hadithi Fikra

Hadithi Fikra Elimika, Burudika pia Sisimuka na Sadari Kisesa...

MWANDISHI/MTUNZI: SADARI KISESASIMULIZI FUPI: HAPPY BIRTHDAY...“Alimjali akampenda k**a ajipendavyo, hakuthubutu na wala...
16/05/2021

MWANDISHI/MTUNZI: SADARI KISESA
SIMULIZI FUPI: HAPPY BIRTHDAY...

“Alimjali akampenda k**a ajipendavyo, hakuthubutu na wala hakujenga chuki zidi yake kwasababu ya upendo. Aliendelea kumpenda kiasi kwamba, hakutaka hata punje kusikiliza maneno ya washambenga wanaouma na kupuliza. Nahisi ni ulimbukeni wa mapenzi mpaka ukampelekea kuwa k**a kiziwi, k**a lahasha! aliwekewa kinyunyizo cha huba kidogo kwenye kinywa. Mh...maana si kawaida kwake kumganda mwanamke kiasi kile k**a ulimbo, na hakuzoeleka vile. Alizoeleka kuwa ni kijana mwelevu mwenye msimamo wa kupenda na kujali familia yake, ila siku kadri zinavyokwenda taratibu alibadilika akawa Kinyonga. Alianza kuchukia familia yake na kuanza kugandisha mawazo mgando kwenye ubongo wake, kwa kufikiria kuwa familia yake inahitaji kumgombanisha na kipenzi chake. Ambaye sasa ni mkewe wa ndoa aliyeoa mwaka kenda bila matarajio, baada ya kupandikiza mbegu na kuzaa matunda kwenye tumbo la mlimbwende wa kisukuma. Hapo alivunja mahusiano na familia yake mwishowe akahama kwenye nyumba ya wazazi ambayo alikuwa akiishi na mkewe, aliondoka mkoani kwao Songea akaelekea Dar es salaam kuanza maisha ya kujitegemea kwenye jiji la Wazaramo. Kinangananga hapa nilikuwa nikimzungumzia Chota jinsi alivyompenda mkewe Zombeta kuliko chochote katika dunia hii, kiasi kwamba mapenzi yao yalikuwa yakilandanishwa na mapenzi yale ya Romeo na Jullieth. Hapa ngoja ninukuu misemo ya wahenga, wahenga walisemaga; “Tembea uone pia, mjini ni shule”.... Hii leo misemo hii ameiamini Chota baada ya kufika kwenye jiji la Dar es salaam na, kuishi kwa ndugu wa mkewe pamoja na mkewe. Polepole maisha ya Dar es salaam yalizidi kusonga hatimaye Zombeta alibadilika sana, hakubadilika sura tu bali alibadilika mavazi mpaka kitabia. Zombeta yule wa Songea alikuwa si huyu wa Dar es salaam, alishawishika mno mpaka akawa anavaa vigauni vifupi venye mpasuo kuntu wenye kuonyesha baadhi ya maungo. Akawa anavaa vipedo na vitopu ambavyo venye kuonyesha kitovu kizuri kilichoingia ndani mfano wa shimo la Panya, hayo yalikuwa mabadiliko ya mavazi tu ya kutoka kwenye magauni marefu ya kujistili mwili. Mpaka kwenye magauni mafupi na vipedo ambavyo vinajenga msisimko washawasha kwa wanaume wa kila walionja balehe.... Upande wa tabia sasa ilikuwa kichekesho, Zombeta huyu aliyekuwa akikung'uta mabega akikataa starehe kule Songea. Ndiye huyuhuyu alipowasili Dar es salaam starehe za kila aina alizimaliza, sio ya kwenda club kwaajili ya kujirusha muziki wa kizazi kipya na sio ya kunywa pombe kali zinazoyumbisha kichwa kwa wasaa mchache tu ukawa chakari.

“Zombeta, mke wangu...hii tabia ya kurudi nyumbani usiku giza totoro ukiwa chakari. Itaisha lini?.... Halafu huoni aibu k**a hapa ni pa watu tumepewa hifadhi kwaajili ya kujistili kwa muda. Hebu...kuwa na aibu kidogo mke wangu,” Chota alijitahidi kukumbuka siku moja maneno ya miezi mitatu nyuma aliyomwambiaga mkewe mara baada ya kuwasili Dar es salaam na kukaribishwa na wenyeji wao vema, wakati huo akiwa sebuleni amekaa kwenye kiti.

“Heeeeeh!!, wewe mwanaume koma...siku hizi wewe ndiye wakunihubiria na kunipangia wasaa wakurudi.... Mimi ndiye wakujipangia nirudi wasaa gani...eti unasema; uoni aibu k**a hapa ni pa watu. Umesema hivo kwani mimi ni mnyama sipaswi kuishi hapa nina mapembe. Hebu...chunga kauli yako mapema kabla sijakurudisha Songea kuchanyachanya mikeka. Oh ooooh!!,” Chota akiwa palepale sebuleni akiwa amekaa kwenye kiti kilichokwisha kwa kuchakaa foronya, aliendelea kukumbuka mpaka lile jibu la karaha alilojibiwa na Zombeta mara baada ya kuhoji kwa shanadhari.

Alifahamu Zombeta atakuja kubadilika tabia ila wapi ndiyo kwanza tabia ikaambatana na kejeli maradufu, kejeli alionyesha kwa mumewe wa ndoa na kwa waliompatia hifadhi ya kuegeza mbavu. Wakati wote hakuvaa mavazi mafupi pekee na hakunywa pombe kali pekee bali, alikuwa anadanga wanaume kwa mkupuo k**a abiria apandavyo daladala bila kujali. Tabia ile Chota alivuta subira ila heri ikaambaaambaa rohoni ikaondoka, alibaki akiumia sana lakini ndiyo atafanyaje na mkewe anamhitaji. Ikabidi ajitahidi kupiga moyo konde na kuweza kuvuta subira kwa mara nyengine kwa vituko afanyiwavyo na mkewe, japo vilizidi kukaanga roho na roho ikaivaa nyongo alizidi kujimaliza kwa kujibebisha ili mkewe amfikirie lakini wapi.... Mbaya zaidi anashikwa na uchungu wa hasira akikumbukaga happy birthday, hii siku yake ya kuzaliwa ilimuumiza sana baada ya kurudi nyumbani akiwa na furaha moyoni. Huku akiwa amebeba keki kwaajili ya kusheherekea siku yake ya kuzaliwa pamoja na mkewe, pozi lake lote lilikwisha baada ya kufungua mlango wa nyumba bila kubisha hodi wanayoishi pamoja na mkewe. Alichokiona ilikuwa ni siri yake na hakutamani kabisa kukiona na hata alipokiona akatamani kuchukua maamuzi ambayo si sahihi, aliona Zombeta akiwa yupo amekaa kwenye kiti kimojawapo kilichopo sebuleni. Akiwa amepakatwa na kuchombezwa mabusu moto na mwanaume ambaye bonge kiasi, mrefu wa wastani mwenye mzuzu kiasi kwenye kidevu. Papohapo Chota akili zake zilihama, macho yake yalimtoka pima na nguvu zilimwisha akaanza kutetemeka mwili mfano wa mgonjwa mwenye pepopunda. Ghafla kablasha la keki alilolishika kwenye mkono wa kuume lilimdondoka likadondoka kwenye sakafu hatimaye alifuata yeye kudondoka kwenye sakafu mfano wa furushi, palepale punde alipoteza uhai baada ya presha yake kupanda na kuanza kuhema kwa tabu mfano wa mtoto mwenye gonjwa la pumu. Alitapatapa na roho pale sakafuni ila aliyekuwa akimjali na kumsikiliza hakuwepo, mkewe alichukuana na bahasha akaongozana na kikwaru wakahama mkoa baada ya kugundua Chota tayari kashaaga dunia.”

“Neno HAPPY BIRTHDAY katika mahusiano yoyote lina maana kubwa sana, kwakuwa linakukumbusha siku ile ambayo uliyokuwa umezaliwa bila kujitambua. Happy Birthday itakufurahisha sana na itakusababisha ujimwambafai...kwasababu itakukutanisha na ndugu, jamaa na nyonga mkalia ini. Usiombe mahusiano yako yakaingia shubiri wakati wa Happy Birthday, maana utaiona siku ni mbaya na kilio kitakuwa rafiki kila uchwao baada ya kukanwa na wahubani mbele ya umati. Naomba thamini sana Happy Birthday ya mwenza wako, maana hiko ndicho kipaumbele kitakachosaidia mahusiano yashamiri na kuwaacha mkijipongeza kwa tabasamu kwenye bustani ya huba.”

MWISHO.

MWANDISHI: SADARI KISESASIMULIZI FUPI: KISANGA CHA MWANDISHIANZA NAYO...“Alizaliwa Kigoma akaishi Kigoma ndipo nyumbani ...
04/03/2021

MWANDISHI: SADARI KISESA
SIMULIZI FUPI: KISANGA CHA MWANDISHI

ANZA NAYO...
“Alizaliwa Kigoma akaishi Kigoma ndipo nyumbani Kigoma, alisoma mpaka elimu za ngazi ya juu akahitimu na akapata stashahada yake safi. Alisaidia kazi za wazazi za kilimo takribani mwaka mmoja huku akijaribu kila pahala kutafuta ajira, kwa juhudi zake za kutafuta kazi kwa njia ya mtandao alikuja kupata kazi katika kampuni kubwa mojawapo iliyopo jijini Dar es salaam. Aliwaaga wazazi na akapokea baraka za wazazi akasafiri kwenda Dar es salaam kikazi, kampuni yake iliwapenda na iliwatii sana wafanyakazi wake hivyo alivyowasili Dar es salaam hakupata tabu yoyote kwakuwa alikuta kila hitaji muhimu kwake aliandaliwa na kampuni. Yeye k**a mfanyakazi wa kampuni ya uzalishaji wa nafaka mbalimbali iitwayo SONDA FOOD'S inayopatikana kwenye nchi mbalimbali ila kwa Dar es salaam inapatikana Mbagala...alipatiwa nyumba nzuri ya kuhifadhi mbavu zake, alipatiwa gari zuri la kutembelea na kuonyesha mikogo yake ya kimanyema mbali na hivyo pia alifunguliwa akaunti ya benki na meneja yenye mkwanja kiasi wa kukidhi mahitaji yake binafsi. Watu wana nyota zao bwana.... Ila mlimbwende Dorofina toto la kimanyema nyota yake iling'aa sana maana alitokea kukubalika na wafanyakazi wenzake mpaka meneja wa kampuni ile, yote kwasababu ya uadilifu na utendaji wake wa kazi madhubuti anaonyesha kila siku pale ofisini. Licha ya kuwa mhasibu kichuna Dorofina kwenye kampuni ile ya uzalishaji wa nafaka pia, alikuwa ni mwandishi nguli wa vitabu katika nchi yake ya Tanzania na vitabu vyake vilitokea kupendwa sana na watu mashuhuri mpaka viongozi wa nchi yote sababu vilikuwa na maudhui safi na uweledi. Kupitia kazi yake hiyohiyo ya uwandishi alitokea kuwa na mashabiki wengi na alikuwa anakutana na watu mbalimbali kwaajili ya kujengana kimawazo na kushauriana mambo ya kimaendeleo, simu yake ya mkononi ilikuwa haikauki jumbe wala kupigiwa na watu mbalimbali anaowafahamu na asiowafahamu kwake aliona ni kawaida tu. Ila siku ya mapumziko ambayo ni Jumapili simu yake iliita sana ilikuwa ni namba ngeni ila hakupokea ndipo ikaingia jumbe ambayo ilimshtua mapigo ya moyo yakaenda kasi na hofu ikamjaa mwili mzima, ujumbe ule ulikuwa ni wa vitisho ambao ulisomeka kwa maandishi makubwa;

“MWANDISHI HUKO UNAPOELEKEA UNAPOTEA....KATIKA FASIHI YAKO ANDIKA MAMBO YOTE YA ULIMWENGU ISIPOKUWA SERIKALI. UKIENDELEA KUKASHFU SERIKALI KWA FASIHI YAKO SAFARI HII KIFO HALALI YAKO.”

Ujumbe ule ulimwogopesha sana Dorofina, wakati huo alikuwa anaandaa kitabu chake kingine kilichokuwa kinaitwa PRESIDENTS DEVIL'S kupitia kifaa chake cha kuandikia fasihi kiitwacho PC aina ya IPhone. Ujumbe ule ulimjengea uwoga mpaka hakutaka kuthubutu kukiandika tena kitabu chake hicho, ulimwogopesha sana kwasababu kitabu chake kile cha safari hii kinakashfu tena serikali ya viongozi wa juu. Ila ndio atafanyaje k**a pesa bado anahitaji, kukuza jina lake bado anahitaji na kupata hasara kwaajili ya fasihi haitaji ikabidi akitoe tu hiko kitabu lakini kwa kuapa kuwa hiko ndiyo kitabu chake cha mwisho kitakachohusu serikali. Alikiandika vivyohivyo akakipitisha kwa mhariri akihariri kikahaririwa, alikipanga kurasa hatimaye akapeleka kwa wachapaji wake wakakichapa kitabu hiko kimazengo. Kitabu kilitoka na kikauzika kila mkoa, kila mji na kila nchi kikapendwa sana na vijana mpaka wazee. Kitabu chake hiki Dorofina alitoa nakala mia tano na katika nakala mia tano vyote vikaisha hakikubaki hata kimoja hivyo alipata faida sana na aliingiza pesa nyingi sana kupitia kitabu chake kile kiitwacho Presidents Devil's, kitabu kile cha mwandishi Dorofina kilisomwa na watu wengi sana kutokana na maandishi yaliyomo mule kubeba jumbe nzito kuhusu serikali. Kilivutia kwa watu wengi mpaka mwandishi mwenyewe akawa anatafutwa kwa udi na uvumba na watu waliosoma kitabu hiko kwa lengo la kumpongeza na kumpa bakshishi, lakini katika watu haohao wanaomtafuta walikuwamo watu wa serikalini. Watu wa serikali walimtafuta mwandishi Dorofina kwa lengo moja tu sio kumpa pongezi wala kumpatia bakshishi bali walikuwa wanamtafuta kwaajili ya kumpatia haki yake aliyokuwa akistahili kupewa tangu awali.

“Hallo,” Dorofina alisema huku akitahamaki mara baada ya kupokea ile namba ngeni kupitia simu yake ya mkononi iliyompigia, wakati usiku ule akitoka kazini na kwenda nyumbani kwaajili ya kupumzisha akili.

“Dorofina.... Ujumbe wetu wa mwanzo uliuona na ukausoma?,” Mtu yule mwenye sauti ya kiume na nzito alihoji mara baada ya kuona mwenye simu aliyempigia amepokea simu na anamsikiliza.

“Yah, niliuona na nikausoma.”

“Sasa ukachukua maamuzi gani?.... Ya kutoa kitabu kingine cha kashfa kinachotuhusu sisi?.”

“Hapana, sikuhitaji kukitoa hiko kitabu. Ila taarifa yenu niliipata angali kitabu hiki kishafika hatua ya mwisho ya kukitoa.”

“Kwanini, haujakizuia kisitoke?.”

“Niliogopa kuingia hasara,” Dorofina aliongea wakati huo akiwa kashawasili katika lango lake kuu la kuingilia ndani lakini alikuwa bado hajaingia ndani akasimamisha nje ya nyumba usafiri wake gari aina ya Crown nyeusi yenye kioo kisichoonyesha “Tinted”.

“Haaah, haaaah, haaaaaah,” Mtu yule kwenye kiwambo cha simu alisikika akiangua kicheko k**a mwehu kisha akakata simu.

Dorofina hajaweka simu yake anapostahili kuweka mara akasikia watu wakigonga kwa nguvu mlango wake wa gari upande wa kwa dereva alipo, wasiwasi ulimjia moyo wake ukadunda pah! k**a kitenesi. Mwili wote ulimtetema mpaka akashindwa kushusha kioo cha gari lake kwa inavyostahili, alishusha kioo cha gari lake kwa wasiwasi huku mkono ukisitasita. Alipofungua kioo mpaka mwisho ndipo akakutana ana kwa ana na vijana watano waliovalia suti nyeusi yenye kizibao cheusi kwa ndani ya suti, na usoni waliovalia miwani isiyoonyesha macho yao vijana wale miili yao ilishiba ikafumuka mithili ya masikio ya Tembo. Mikono yao ilijazia haswa na walikuwa wamepanda hewani mithili ya Twiga kwa muonekano wao tu mtu ujiulizi mara mbilimbili utakuwa ushapata jibu kuwa wale walikuwa ni mabausa ndiyo wametumwa na serikali kwaajili kumpatia Dorofina haki yake anayostahili kupata, walimteremsha mlengwa wao kwenye gari mkukumkuku au msobemsobe wakamweka kando ya gari lake wakampiga kipondo cha Mbwa mwizi kisha wakamlawiti kwa kufanya nae tendo kinyume na maumbile na kinguvu yaani walimbaka. Bausa zote tano zilimbaka mwanamke mmoja ambaye ni mnyonge hatimaye wakatokomea wakamwacha Dorofina akiwa chini damu nyingi zikitoka sehemu husika na huku akiwa anatembelea tumbo k**a Nyoka na huku akiugulia kwa maumivu ayapatayo kwenye mapaja na sehemu husika, kwakuwa pale alipoteza damu nyingi na hakuna msaada wowote uliotokea ghafla akanyongea akawa mpole mwishowe akajihisi kizunguzungu na palepale nguvu za mwili polepole akahisi zikiisha papohapo akaaga dunia.

“Kabla ya yote ukihitaji kufanya kitu kwanza fikiri kabla ya kutenda, ukishaona kitu unachotaka kufanya ni sahihi anza kuthubutu kisha fanya.
Usikurupuke maana hata mvumo wa upepo unakurupuka lakini unakuja kutulia na kunyongea bila habari, wewe fanya mambo yako bila makosa tu hapo ndipo utakapoona dunia umeiweza.
Utakuwa dunia umeiweza sio kidogo utakuwa umeiweza sana, na matunda yake utayaona tu yatakavyokudondokea miguuni utakuwa kazi yako sasa ni kula huku ukicheua furaha.”
MWISHO.

MWANDISHI: SADARI KISESASIMULIZI FUPI: KIFO CHA ZONGOSOMA...“Hello...mama yangu kipenzi.”“Hallo...mwanangu kipenzi, tege...
04/03/2021

MWANDISHI: SADARI KISESA
SIMULIZI FUPI: KIFO CHA ZONGO

SOMA...
“Hello...mama yangu kipenzi.”

“Hallo...mwanangu kipenzi, tegemeo langu na kimbilio langu.... Hujambo?.”

“Sijambo mama...vipi hali yako inaendelea vizuri? na dawa zako mpaka sasa ushakunywa?.”

“Mwanangu. Ugonjwa wangu nafikiri unaujua hautabiriki saa yoyote nipo sawa na saa yoyote sipo sawa.... Kuhusu dawa nasubiri nipate chakula cha mchana tu ndio ninywe hizo dawa zangu.”

“Aisee!!....inamaana mpaka sasa mama ujanywa dawa zako. Angalia saa tisa alasiri hii inakwenda saa kumi jioni uoni k**a hatari kwa afya yako.... Halafu kumbuka mimi natafuta pesa kwa uvumba kwaajili yako mama uweze kupata chakula kwa wakati na dawa zako kwa wakati. Usifanye mzaha kabisa na maradhi.”

“Eeeeh, basi mwandishi wangu usiwe Mbogo. Ni leo tu dada yako kachelewa kuandaa chakula naamini halitojirudia hili kosa la leo.”

“Bora iwe hivyo, maana sipendi kabisa mtu afanye mzaha na afya yake mwenyewe.”

“Basi sasa mwandishi eh. Ukianzaga kuongea unatakaga mpaka misuli ya kichwa ichomoke itoke nje jamii wote waione, tumekuelewa.... Halafu vipi hali yako huko Dar es salaam?, vipi kuhusu kazi yako unaendelea nayo vema? na vipi wafanyakazi wenzako na meneja wako wa HOTRO PUBLISHER'S COMPANY unaishi nao na unafanya nao kazi kwa upendo?.”

“Mama huku hakuna upendo. Wafanyakazi wenzangu wananionea kengeza baada ya kuona hadithi zangu karibia zote zinapendwa kwenye magazeti ya kampuni yetu na meneja wangu kwasasa aniamini kabisa anahisi natembea na mke wake mtarajiwa.... Mama, kuendelea kufanya kazi katika kampuni hii siwezi, mimi naondoka bora nikafanye kazi kwengine tu wasije binadamu hawa wakaniletea kisanga mwishowe waniue kabisa.”

“Eeh!!, eeeeh!!!...k**a ni hivyo mwanangu ukiona mambo magumu sana huko Dar es salaam rudi nyumbani. Huku ujaua rudi tu na kuhusu ugonjwa wangu wewe usifikirie sana ikiwezekana achana nao.... Nishampoteza baba yako katika dunia hii, kwasasa wewe sihitaji kukupoteza yaani...kwangu wewe ni thamani kuliko chochote.”

“Mama kurudi kwasasa sitorudi nyumbani. Mimi ni mwanaume siwezi kata tamaa kirahisi acha nikajaribu kufanya kazi katika kampuni nyengine...k**a kampuni huku Dar es salaam zipo nyingi sana siwezi kukosa kupata kazi hata kwenye kampuni moja. Najaribu.”

“Sawa k**a umehamua, jaribu tu...mimi sina kipingamizi kwako maana ushakua libaba unajielewa, mimi nitabaki nikikuuthudu katika maisha yako.”

“Nashukuru mama, ila nisikuchoshe pumzika kidogo nilikuwa najulia hali ya afya yako tu. Pia usisahau utakapokula tayari kumbuka kunywa dawa zako.... Bye” ilikuwa ni sauti ya upole iliyokuwa ikisikika kwenye kiwambo cha simu ikimwaga mama yake mzazi. Ilikuwa imejaa ucheshi na ilikuwa inatoka kwa uzuri kwenye kinywa cha kijana mmoja mwenye kipawa cha uwandishi wa hadithi.

Mwandishi huyu wa watu alijulikana kwa majina ya Zongo Korongo, jina ambalo amepatiwa na wazazi angali mdogo na sasa kashakuwa mkubwa anaendelea kudumisha jina lake hilo. Alilidumisha jina lake kila nyanja kwa kupitia hadithi zake ambazo zinaandikwa sana kwenye magazeti ya kampuni yao, magazeti ndiyo yaliyomkuza haswaa mpaka kupelekea kufahamika na kila rika linalotoka nchi mbalimbali mpaka za ughaibuni. Kufahamika kwake ilikuwa ni furaha na alijimwambafai sana kwenye nafsi yake na kwa mama yake, lakini kwa wafanyakazi wenzake ambao anafanyaga nao kazi pale katika ofisi moja na kampuni moja kwao haikuwa furaha walijenga chuki rohoni mwao wakazipalilia na wakazivuna haswaa kwa kutompenda. Umaarufu wake na ugalacha wake wa kuandika hadithi za kuelimisha na kusisimua ndipo zilipozaa matunda kwa kupendwa na mke mtarajiwa wa bosi wake ambaye ndiye meneja wake anayemsimamia kwa kila kitu katika maisha, alitongozwa na hakuweza kukataa kwasababu kuhofia kibarua kuota nyasi hivyo mahusiano yake na mke wa bosi yalitaradadi japo yalikuwa mahusiano ya kisiri. Wanasemaga kuwa mapenzi ya dhati sio siri mtajificha kwa kuibia ila ipo siku uvumilivu utawashinda mtataka ikiwezekana dunia yote ijue kwa jinsi mnavyopendana, ndivyo yalivyotokea kwa Zongo. Yeye alitaka kuwa huru na alitaka mapenzi yasiyo ya siri k**a hapo awali, alijitanua mwanaume kwenda kila nyanja na mlimbwende mzuri kwaajili ya kula bata tu na sio kingine...kwakuwa kila alichokuwa anataka alikuwa anatimiziwa na mke wa bosi basi alijisahau akaona dunia kaipatia hakujali k**a yule ni mali ya mtu na akufikiria k**a alichokiona chaelea kimeundwa, mahusiano yao ya hadhara hatimaye bosi alikuja kupata taarifa kuwa mkewe mtarajiwa anatoka kimahusino na kijana wake wa kazi. Dunia siku zote haina siri, bosi taarifa hizo alizipata kwa mmoja wa rafiki zake ambaye aliyekwenda kuponda mali katika hoteli mojawapo hapa Dar es salaam iitwayo Rozoka ndipo alipomwona shemeji akiwa amekumbatiwa na mwandishi Zongo kwa huba. Taarifa zile hazikuchuliwa juujuu bali zilichunguzwa kwanza kabla maamuzi ayajatendwa, bosi alipojiridhisha kuwa taarifa zile ni za kweli hazina figisufigisu alihamua kumuua Zongo mwenyewe kwa mikono yake mwenyewe kabla ya Zongo kushtuka na kwenda kutafuta kazi kampuni nyingine. Yeye ni mtu mkubwa bwana hivyo bastola kwake sio cha kuuliza alikuwa anayo, alimuua Zongo kwa bastola yake ndogo nyeusi na hakumuua Zongo pekee kwa bastola bali alimuua mpaka mke wake mtarajiwa wakati alipowakuta Zongo na mkewe siku hiyo kwenye nyumba za kulala wageni ambayo iliyokuwepo katikati ya mtaa wa uswazi wa Manzese. Alifanya mauaji kisha yeye papohapo akak**atwa na polisi akapelekwa rumande kunyea debe na kula chakula cha bure cha serikali, alikwenda gerezani lakini akiwa mtu mwenye huzuni pindi akumbukapo ukata aliowacha uraini. Huzuni yake ilikuwepo lakini huzuni ya Mama Zongo ya kuondokewa na mwanae kipenzi hapa duniani ilikuwa maradufu, alilia baada ya kupokea taarifa za kifo cha Zongo hakulia kidogo alilia zaidi na zaidi mpaka mwili wake ukanyong'onyea ukawa mdogo mfano wa kidonge cha mafua kiitwacho Pritoni. Nikisema alilia zaidi haitoshi alilia mpaka macho yakawa mekundu na kuzimia mara tatu ya nne hakuamka kabisa alikwenda mazima akafa akaonja umauti.

“Najua unapitia mazingira magumu kupata mkate wa kwenda kinywani, lakini licha ya mazingira magumu uliyonayo haikupasi kuchukua au kuiba mali isiyo yako.
Ni mwiko kuchukua au kuiba mali isiyokuwa halali kwako maana uarabuni utanyongwa k**a sio kuchinjwa k**a Kuku, sasa ya nini yote ya kukumbe angali wewe sio kipofu upo kamili kila idara nakusihi katika maisha penda kujikwamua hapo ndipo kesho ahueni k**a sio leo.”
MWISHO.

MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI                SEHEMU YA TANOWalipomaliza kula Sharifu akatoa vyombo akaenda chumbani na kumwa...
02/03/2021

MAMA USINIFUNDISHE UCHAWI

SEHEMU YA TANO
Walipomaliza kula Sharifu akatoa vyombo akaenda chumbani na kumwacha mama yake kwenye mkeka pale ukumbini akishona khanga. Safari hii Sharifu hakutaka kusikiliza redio, alipofika kitandani akajitupa chali na kujibembeleza kwa kujitingisha miguu punde tu akapitiwa na usingizi.
Alikuja kushtuka mishale mingine kuchungulia dirishani akaona giza limetanda pande zote kuashilia usiku umeingia huku likisindikizwa na wingu zito la mvua na mweku mweku zikimurika na kuzima kuwa giza. Hali ile kwa mtu muoga asingethubutu kunyanyua miguu yake na kutoka nje.

“Giza hili, naona linaniruhusu kwenda kilingeni ngoja nikamwamshe mama,” Sharifu alijisemea nafsini kisha akajibadilisha muonekano akayayuka chumbani kwake na kutoka nje kuelekea kwenye mlango wa chumbani wa mama yake na hatimaye kuongea kwa hisia na mama yake.

“Amka mama.”

“Naona leo umewahi sio kawaida yako, ama kweli umepania,” Binti Mngane aliongea naye huku akijibadilisha muonekano mara baada ya kuamka.

“Ninashauku sana na wamama wale, si wanajifanya wanajua sasa leo watakiona cha mtema makuni,” Sharifu alizungumza huku akizungusha macho yake kimiujiza.

“Kweli dhahiri, umewapania.”

“Wewe, acha tu mama,” Sharifu alimsubiri kwa muda mama yake, ghafla akamuona mama yake ametokea kimiujiza alipo yeye. Akiwa tayari kashajiandaa wakayayuka pamoja tayari kuanza safari na kabla ya kufika kwenye tukio wakashauriana.

“Unavyoona wewe, tuanze wapi?,” Binti Mngane akauliza.

“Naona k**a vile kwa Mama Abuu ni karibu tuanze kwake, baadae tukishatoka kwa Mama Abuu ndiyo twende kwa Mama Stumai,” Sharifu alimjibu mama yake huku akitupa usinga huku na kule kwaajili ya kusafisha njia.
Waliposhauriana na mama yake wakaelekea moja kwa moja kutua kwenye uwanja wa nyumbani wa Mama Abuu. Walipotua wakashangazwa sana na hali waliokumbana nayo, wakakuta zizizi kumetulia huku kukichochewa na giza. Hali ile tulivu ikawafurahisha sana.

“Inaonekana Mama Abuu yupo kwenye usingizi mzito, lengo letu tulifanye haraka tuondoke,” Binti Mngane alimweleza mwanae huku akiusogelea mlango wa kuingilia ndani.

“Basi niache niingie ndani, kinachojiri nitakujuza,” Sharifu alimwambia mama yake huku akiegemea mlango wa Mama Abuu na kuyayuka kutokea chumbani.
Sharifu akamkuta Mama Abuu yupo kitandani amelala na mumewe usingizi wa pono. Akamchukua kimazingara mtuhumiwa wake na kutoka naye nje. Binti Mngane alipomuona mwanae amerudi na Mama Abuu kwa kumkokota k**a mkokoteni akafurahi sana.

“Naam!!!, huo ndiyo uwanaume,” Binti Mngane alimsifia mwanae mara baada ya Sharifu kufika alipo.

“Mtu wetu, huyu hapa,” Sharifu aliongea huku akimkabidhi Mama Abuu kwa Pilato.
Alipokabidhiwa kwa Binti Mngane akamwagiwa unga mweupe wa chengachenga unaofanana na mchanga unaosaidia mtu asiweze kuamka mapema. Akiwa hajitambui wala kuonyesha dalili ya kufumbua macho akawapa moyo na kuwafurahisha Binti Mngane pamoja na mwanae.

“Huyu mtu inaonyesha dawa tuliyompatia, itatufanya tufanye kazi yetu bila kipingamizi,” Binti Mngane alimwambia mwanae huku akipanda tumboni mwa Mama Abuu aliye na ujauzito wa miezi nane.

“Umejuaje?,” Sharifu aliuliza huku akimkodolea macho mama yake.

“Nimeona kuwa Mama Abuu, hana kinga.”

“Kwa hiyo tutafanikiwa, kufanya kazi yetu kwa uzuri,” Sharifu aliongea kisha kwa pamoja wakafurahi na mama yake huku wakicheza kwa kukata viuno kwa maringo.
Baada ya muda kadhaa Binti Mngane akafungua kitambaa cheusi kisha akatoa kimzizi chenye miiba mikali. Akakitemea mate kimzizi kile hatimaye akamlisha kinywani Mama Abuu. Walipohakikisha wamemaliza kumlisha kimzizi wakamrudisha Mama Abuu chumbani aendelee na usingizi.

“Mama Abuu dawa yake ipo jikoni inachemka, baada ya muda mfupi atainywa,” Binti Mngane alimweleza mwanae mara baada ya kumrudisha Mama Abuu.

“Nikiwa nawe nafarijika na kujifunza, mambo mengi sana mama yangu.”

“Yakupasa ujifunze mengi tunayofanya, ili baadae uweze kuwa mwanachama madhubuti,” Binti Mngane alimweleza mwanae huku akinusisha pua kila upande ajue k**a kupo shwari.

“Nitajifunza kila kitu kutoka kwako...lakini mama muda ushakwenda twende kwa Mama Stumai sasa tuk**alize kazi yetu,” Sharifu alimwambia mama yake mara baada ya kuona wanachelewa kwenda kwa Mama Stumai.

“Kweli tuondoke, tusije kuchelewa tukaumbuka kukipambazuka,” Binti Mngane safari hii alinusa juu ya anga kisha akamshika mikono mwanae na kuyayuka eneo lile.
Binti Mngane na mwanae wakaelekea nyumbani kwa Mama Stumai. Hali ya hewa kwa wakati ule ilionyesha anga ikiwa na mwanga hafifu huku nyota zikiendelea kumelemeta kwa mbali ikiashilia kuwa kunakaribia kupambazuka.

“Tushafika sehemu husika, nisubiri nje safari hii mimi niende nik**alize mchezo,” Binti Mngane alinong'ona mara baada ya kutua kwenye uwanja wa Mama Stumai.

“Ila kuwa makini, si unajua madhara ya hii nyumba?,” Sharifu aliuliza kwa kumhabarisha mama yake.

“Madhara gani tena? mbona unanitisha,” Binti Mngane aliuliza kwa kutaka kujua madhara ya nyumba ile.

“Wewe ushasahau, k**a Mama Stumai ni mrokole?.”

“Mmh!!! nilikuwa nimeshasahau, nitakuwa mwangalifu usijali kuhusu hilo mwanangu,” Binti Mngane alisema huku akienda ndani kinyume nyume mara baada ya kufungua mlango.

“Sawa, nitakusubiri,” Sharifu aliongea huku akizunguka nyumba ya Mama Stumai kwa kusota makalio kuhakikisha usalama.
Binti Mngane alipokaribia mlango wa kuingia chumbani mwa Mama Stumai akasotea mlango kwa makalio hatimaye mlango ukafunguka kisha akaingia chumbani. Alipofika chumbani akamkuta Mama Stumai akiwa amelala nafasi ile Binti Mngane hakutaka kuichezea.

“Wewe si mjanja!. Sasa leo nakuonyesha k**a kuna wajanja zaidi yako,” Binti Mngane alijisemea moyoni kwa kumtupia vijembe mzazi mwenzake.

Baada ya kutupa vijembe hakuchelewesha akanyoosha mkono wa kushoto mbele kisha likatokea pembe la ng'ombe.
Akampiga Mama Stumai miguuni na lile pembe, alipoona k**aliza mchezo bila kipingamizi chochote akajipongeza kwa kicheko hatimaye akayayuka pale chumbani na kutokea nje alipomwacha mwanae.

“Sasa kazi imekwenda vizuri bila kuchelewa tutoweke eneo hili kabla akujapambazuka,” Binti Mngane alimwambia mwanae kisha wakaondoka na kuja kutua kwenye uwanja wao wa nyumbani na kila mmoja akaingia chumbani kwake kujipumzisha kwaajili ya kuondoa uchovu.

**********
Asubuhi ya alfajiri mume wa Mama Abuu akawahi kuamka kwaajili ya kuwahi shamba k**a desturi yake ya siku zote, lakini alivyoamka akashangazwa na jambo aliloliona kwa mkewe.

“Wewe Siawezi,” Baba Abuu alimwamsha mkewe kwa kumpiga vibao.

“Kuna nini, Chang'ari?,” Mama Abuu aliuliza akiwa bado usingizini.

“Tumbo umelifanyaje?,” Baba Abuu alifoka na uso kaukunja k**a Nyati.

“Kwani lina nini?,” Mama Abuu aliuliza na hakuelewa mumewe ana maanisha nini kutokana kuwa alikuwa bado anaendekeza usingizi.

“Mtoto wangu wa tumboni umempeleka wapi?..ushaenda kumtoa kafara nini?,” Baba Abuu aliuliza kwa sauti ya juu huku akionyesha kuwa na hasira.

“Mungu, wangu!!!,” Mama Abuu alishtuka toka usingizini mara baada ya kuona ujauzito wake kupotea. Kisha akameza mate kwa muda na kumtazama mumewe aliyefura k**a mzoga wa Bata na kulijibu swali aliloulizwa.

“Mimi sielewi kitu,” Mama Abuu alijibu huku akijiangalia tumbo lake mara mbili mbili asiweze kuamini kilichotokea.

“Wewe mwanamke usinifanye sina akili, nina akili zangu timamu niambie mtoto yupo wapi?.”

“Sijui Chang'ari.”

“Nakuambia hivi kuanzia sasa sihitaji kukuona katika nyumba yangu mpaka pale utakapomrejesha mtoto wangu. Mwanamke gani unaendekeza ushirikina,” Baba Abuu alimfukuza mkewe kwa kumvuta atoke nje huku akimpiga ngumi za tumboni mara baada ya kuona mkewe mbishi kutoka ndani. Hakumsikiliza kabisa mkewe, akamfukuza mkewe k**a Mbwa aliyemlia mboga ya ngama.

**********
Mama Stumai akaamka asubuhi akiwa na furaha tele, lakini furaha yake ikaja kuzizima bila kutarajia mara baada tu ya kunyanyua mguu wake wa kuume na kuona umepooza.

“Looh!!!, nini tena hiki?,” Mama Stumai akajiuliza.

“Siamini, mbona haya maajabu nilale mzima niamke nimepooza,” Mama Stumai alijisemea huku akijikokota kushuka kitandani na kukaa sakafuni kwaajili ya kujinyoosha miguu athibitishe.

“Nimeamini uchawi upo japo sikuamini mwanzoni, kweli usilolijua ni k**a usiku wa giza,” Mama Stumai alizidi kusema na kujuta pale sakafuni. Furaha yake yote ikapotea kwa siku ile na punde tu akajikuta mwenye msongo wa mawazo. Akashindwa hata kujizuia kutoa chozi na asimuone wa kumfariji kwa nyakati ile ya matatizo kwake.

**********
Binti Mngane asubuhi na mapema akawahi kuamka na kuzifanya shughuli zake za nyumbani. Muda ulikwenda sana akaona mwanae hana hata dalili ya kuamka ndipo ikamlazimu aende kumwamsha.

“Sharifu, Sharifuu” aliita Binti Mngane kwa kupaza sauti.

“Naam!!!,” Sharifu aliitika kwa kukurupuka toka usingizini mara baada ya kuamka na kufikicha macho.

“Kulala gani hadi saa hizi?.”

“Nimechoka mama, niache nipumzike,” Sharifu alijibu kiuchovu kisha akajilaza tena kitandani.

“Mwenye usingizi peke yako, mbona nami nina usingizi ila nimeamka kufanya kazi...ebu nawe amka,” Binti Mngane alimwambia mwanae kwa kumlazimisha aamke.

“Naomba mama niache nilale kidogo. Nikiamka nitafanya hizo kazi,” Sharifu aliomba mama yake amwache alale kisha akavuta shuka akaendelea kulala.

“Lala ila jua, ukiamka kuna kazi zinakusubiri,” Binti Mngane alimuhabarisha mwanae kisha akaenda jikoni kupika. Baada ya masaa kupita Binti Mngane akawa kashaivisha uji na viazi vitamu. Akatenga chakula ukumbini kisha akaenda kumwamsha tena mwanae.

“Wewe, mtoto.”

“Naam.”

“Uji! tayari.”

“Nakuja.”

“Fanya haraka.”

Sharifu akatoka chumbani kwake mara baada ya kuitwa na mama yake huku akipepesuka k**a mlevi wa gongo kutokana na usingizi. Akajifikicha macho ili aweze kuona mbele vizuri. Akajikongoja taratibu hadi ulipo mswaki kisha akauchukua na kuelekea uwani ili kusafisha meno na uso nyuma akimwacha mama yake akimngoja ukumbini.

“Sharifu,” Binti Mngane alimuita mwanae mara baada ya kuona anachelewa kurudi.

“Na naam,” Sharifu aliitika kwa shida kutokana na mswaki kuwa kinywani.

“Huko kunawa, mwaka!.”

“Nakuja, ndiyo nafunga mlango wa uwani.”

“Harakisha bwana, tuje tule,” Sharifu punde tu alirudi ndani na kuketi kwenye mkeka ukumbini mara baada ya kuchomeka mswaki ukutani.
Walipomaliza kunywa uji Binti Mngane akatoa vyombo nje avioshe.
Sharifu akapumzika kidogo kisha akanyanyuka kwenye mkeka na kwenda kufagia banda la kuku. Akafagia huku akijiburudisha wimbo ambao aliwahi kufundishwa na baba yake kipindi cha nyuma kabla ya uhai wake.

“Mdooogo mwanangu mdogo...aowa owa,
Jisomeee mwanangu jisomee...aowa owa,
Uniokoooe mwanangu uniokoe...aowa owa,
Nakuombeeea baba yako nakuombea...aowa owa,
Kwa mwenyeeezi nakuombea kwa mwenyezi...aowa owa,” Sharifu aliimba nyimbo hiyo k**a mara mbili na kucheza kwa kutingisha kichwa na kunyanyua miguu.
Binti Mngane alipomaliza kuosha vyombo akaenda kwenye banda la kuku kumwangalia mwanae k**a anafagia au lah. Kufika akashangaa kuona mwanae akiimba nyimbo aliyoipenda kuiimba mumewe kipindi cha nyuma.

“Leo unafuraha, eenh?,” Binti Mngane aliuliza mara baada ya kufika bandani.

“Sina furaha, yoyote,” Sharifu akajibu.

“Mbona nakuona, unaimba na kucheza kwa furaha?.”

“Najiimbia tu mama yangu, nisichoshwe na kazi,” Sharifu alijibu huku akizoa kinyesi cha kuku na kukiweka kwenye ndoo ya taka.

“Umenikumbusha mbali.”

“Kivipi?.”

“Nyimbo hiyo unayoimba inanikumbusha miaka ya tisini na nne hivi, kipindi alichonioa baba yako alikuwa anapenda kweli kuimba nyimbo hiyo.”

“Kweli?.”

“Eehe!.”

“Nyimbo hii unajua, kanifundisha nani.”

“Sijajua.”

“Kanifundisha baba huyo huyo.”

“Nilijiuliza huyu mtoto nyimbo hii kaitoa wapi, kumbe umefundishwa na baba yako.”

“Eenh...natoka siku hiyo nimetokea kuipenda kweli hiyo nyimbo.”

“Ulikuwa kumbe na baba mzuri sana?.”

“Sana tena sana kwa jinsi alivyokuwa ananipenda baba hadi leo hii angekuwepo nisingetaabika,” Sharifu alijibu kisha akabeba ndoo na kwenda kumwaga kinyesi cha kuku.

Binti Mngane alipohakikisha mwanae amemaliza kufagia banda la kuku alikwenda ndani kukaa kwenye mkeka ukumbini. Sharifu alipomwaga taka akajongea hadi chumbani na alipofika kitandani akajitupa kifudifudi masaa mawili mbele. Sharifu akak**atwa na usingizi mzito, akiwa amesinzia akaingia Mzee Damanda chumbani kwake kimiujiza na kuanza kuzungumza naye kupitia ndoto.

“Kibaraka wangu,” Mzee Damanda akaita.

“Naam” aliitika Sharifu ndotoni.

“Nimekuja, kuna jambo limenileta.”

“Jambo gani?.”

“Umepita mwezi sijawaona kilingeni kulikoni?.”

“Kulikuwa kuna mambo kidogo tunaweka sawa.”

“Unakumbuka katiba yetu?.”

“Nakumbuka.”

“Zipi?.”

“Usimjaribu mwanachama mwenzio. Usitangaze siri za chama na kuhudhuria kilingeni kila siku.”

“Safi...mbona nyinyi mnakiuka katiba?.”

“Tunapitiwa kiongozi wetu...lakini kuanzia leo nakuahidi hatutokosa kilingeni.”

“Sawa...naondoka ila mkae mkijua nisipowaona siku zijazo nitajua cha kufanya.”

“Nimekuelewa kiongozi, kuanzia leo tutakuwa kilingeni pamoja wala hatutokuangusha tena.”
Mzee Damanda alipoondoka, Sharifu akakurupuka ndotoni. Akanyanyuka kitandani akaelekea moja kwa moja alipo mama yake. Akamkuta mama yake ukumbini ameketi kwenye mkeka na hawamu hii akiwa anamenya ndizi.

“Mama,” Sharifu akaita.

“Eeehe niambie...naona umeshaamka,” Binti Mngane aliongea huku macho yake yakitazama chini akichukua ndizi nyingine.

“Nimeamka...lakini nimeamka na habari mbaya” aliongea Sharifu kisha akasimama mbele ya mama yake sawa sawia.

“Kutoka, wapi?” aliuliza Binti Mngane kwa kutahamaki.

“Kwa, Mzee Damanda.”

“Anashida gani tena?.”

“Kaja kutupa onyo kwa sababu hatuhudhurii kwenye kilinge.”

“Mh! ni kweli...sasa wewe ulimwambiaje?.”

“Sikumwambia chochote, zaidi ya kukiri kosa na kuomba msamaha.”

“Nakuasa mwanangu tujirekebishe bila hivyo mwaka huu tutaumbuka.”

Sharifu baada ya kuzungumza na mama yake akamuaga mama yake kuwa anakwenda nyumbani kwa kina Kondo kupiga stori kidogo. Mama yake akamruhusu aende lakini wakati anaanza safari njiani akakutana na bibi kikongwe asiyeweza kutembea kutokana na kuvimba miguu.

“Mjukuu wangu” aliita Kikongwe yule mara baada ya kumuona na kupishana naye Sharifu.

“Naam” aliitika Sharifu kwa busara.

“Naomba msaada.”

“Msaada upi?.”

“Wa kunipeleka nyumbani.”

“Sitoweza bibi kuna mahali nawahi.”

“Naomba unipeleke nitakupa zawadi tukifika nyumbani kwangu,” Kikongwe yule alimrubuni Sharifu kwa zawadi.

“Zawadi ipi?.”

“Wewe nipeleke zawadi hiyo utaiona tukifika,” Sharifu akakubali kumpeleka Kikongwe yule kwake kwa kumbeba mgongoni kwa sababu ya kutoweza kutembea vizuri.

Wakiwa wapo njiani Sharifu akahisi maumivu makali mgongoni. Akapeleka nyuma mkono wake wa kuume kulipo na maumivu ili apate kuthibitisha k**a kweli ana jeraha au laa. Ghafla yule bibi akabadilika kuwa Chui mwenye miguu minne na kumrarua Sharifu mkono alioupeleka nyuma kupapasa.
Sharifu akamtupa pembeni kikongwe yule kwa hasira. Baada ya kutupwa kikongwe yule akawa anacheka kwa sauti ya juu huku sauti yake ikisikika kufika masafa ya mbali.

“Msaada ninaotaka kukupa unaona haufai? Unaamua kunidhuru?,” Sharifu aliongea kwa ghadhabu.

“Lengo langu si msaada kutoka kwako lengo langu ni kukuua,” Kikongwe yule alisema kwa ujasiri uliotukuka. Sharifu akacheka kisha akasema naye kwa ujasiri bila hofu.

“Unajiamini sana...ngoja nami uone nipoje.”

Sharifu muda huo huo naye akabadilika kuwa Simba mwenye pembe ndefu na meno makali mithili ya sindano.
Alipojibadilisha vile tu moja kwa moja akamvamia kikongwe yule aliyejibadili Chui na kupeana mikong'oto ya haja. Mikong'oto ikatembezwa yapata masaa mawili kisha kila mmoja akawa pumzi kisoda. Sharifu hakukubali kushindwa japo alichoka lakini akamkabili vyema kikongwe yule na hatimaye kikongwe yule akashindwa akatafuta upenyo akakimbia. Sharifu akacheka sana na akaongea kwa dharau.

“Ulijua nipo kijingajinga, nina nguvu balaa. Nenda kajipange na nguvu zako za mtoto mchanga.”
Sharifu akahairisha hadi safari yenyewe kutokana na kuchafuka mara baada ya kurudi kwenye hali ya ubinadamu akarudi nyumbani.
Akafika nyumbani akakuta kumetulia na hadi mama yake hakuwepo. Hakuwa na shaka sana, hivyo akaingia chumbani huku moyoni akijiuliza baadhi ya maswali.

“Kikongwe yule katokea kijiji gani?..na lengo la kuniua ni nini?.”

“Mama anaweza kumjua kweli?..looh! simjui hata jina kikongwe yule.”

“Nitamweleza mama kwa maumbile, k**a atamjua anitajie jina lake nimjue.”

Sharifu akiwa yupo kitandani bado akiwa anajisemesha mara usingizi ukamjia na akawa anakoroma bila kujijua. Masaa kadhaa mbele alikuja kushtuka mara baada ya kusikia mlango wake wa chumbani ukigongwa. Akakurupuka kutoka kitandani na kwenda kumfungulia anayegonga.

“Mama ulikuwa wapi?,” Sharifu aliuliza mara baada ya kuona kuwa aliyekuwa anagonga ni mama yake.

“Nilikuwa mtaa wa pili nikiazima p**a la kupikia pombe...si unajua kesho pombe kwangu?,” Binti Mngane akajibu na kuuliza.

“Umelipata p**a lenyewe?.”

“Nimelipata...ila ni chafu kanisaidie kuliosha.”

“Kuna kazi kwa sasa unataka kufanya?.”

“Nataka nifue nguo mara moja maana zimekuwa chafu sana.”

“Sawa...mimi ngoja nikasafishe p**a hilo,” Sharifu baada ya kupeana majukumu na mama yake, kila mmoja akaingia katika kazi yake.
Baada ya saa moja wote wakawa wamemaliza kazi wakaenda kuketi ukumbini kwa pamoja wapige soga. Sharifu akaanzisha mazungumzo mara baada ya ukimya wa mama yake wa muda mrefu.

“Mama, hivi hapa kijijini kwetu kuna bibi vikongwe wangapi?.”

“Wawili,” Binti Mngane alijibu huku akitabasamu.

“Nani na nani?.”

“Bi Kazimoto na Bi Tuni...kuna nini kwani?.”

“Leo njiani, nimekutana na bibi kikongwe akanidhuru.”

“Yupoje, kikongwe huyo?.”

“Miguu yake, imevimba na mfupi.”

“Oooh!, huyo atakuwa Bi Kazimoto.”

“Unamjua?.”

“Eeenh!.”

“Anaishi wapi?.”

“Ni jirani yetu, anaishi nyumba tatu za mbele zinazofuata...alitaka kukudhuru kisa nini?.”

“Sijajua...sio kunidhuru tu, alitaka aniue kabisa.”

“Toba!!!, majirani wananitafuta nini?..ujaumia sana?.”

“Sijaumia sana ameniweka kajeraha kidogo tu...lakini nina hasira naye.”

“Unatakaje?.”

“Kama unapajua kwake, baadaye unipeleke nik**alize hasira zangu.”

“Usijali, baadaye tukitoka kilingeni nitakupeleka,” Binti Mngane alipiga soga na mwanae hadi nyakati za kupika chakula zikafika.
Akanyanyuka kwenye mkeka pale ukumbini na kuelekea jikoni kupika chakula cha usiku. Sharifu hakutaka kuendelea tena kukaa pale ukumbini. Akaamua kuchukua mkeka na kwenda kujilaza nje kwaajili ya kupunga upepo wa jioni.

**********
Nyumbani kwa Bi Kazimoto furaha haikuwepo. Alikuwa anawaza na kuwazua kwa jinsi alivyokosa ushindi.

“Mtoto yule anatumia uchawi wa aina gani?..atakuwa anatumia uchawi wa kale nini?.”

“Yaani kitoto kile kinishinde mimi............? Sikubali nitajipanga tena.”

Bi Kazimoto kwa siku ile ilikuwa ya huzuni kwake na mbaya zaidi kila akifikiria tukio lile. Akahisi homa, yaani hakutamani hata chakula cha aina yoyote kipite kinywani mwake. Yaani siku ile chakula hakikuwa kitamu upande wake hivyo akalala bila kula kitu chochote siku hiyo.

**********
Binti Mngane alipoivisha chakula na kula yeye na mwanae wakaingia kila mmoja kwenye chumba chake kwa ajili ya kwenda kujipumzisha mwili. Binti Mngane akiwa usingizini akazama moja kwa moja kwenye ndoto, ndoto ikampeleka ajione yupo na mumewe wanazungumza.

“Mwanamke mbaya sana, yaani umeniua kwa kunitoa kafara kwasababu ya kunufaisha uchawi wako,” Baba Sharifu alinung'unika kwa kumnung'unikia mkewe kwa kumwaisha kaburini.

“Si kusudi langu, ni kusudi la mizimu kunilazimisha kutoa kafara kinguvu,” Binti Mngane alijitetea ili asionekane mbaya na mumewe.

“Mbona hujamweleza mtoto uchafu uliofanya...halafu unajitetea leo. Lazima nikuue,” Baba Sharifu aliongea na kutaka kupeleka mikono yake kwenye shingo ya mkewe amkabe.

“Tobaaa!!!, roho yangu,” Binti Mngane alishtuka kwa kukurupuka ndotoni huku akihema kwa kasi k**a mwizi aliyekimbizwa na raia.

Sharifu kwa makelele ya mama yake akashtuka usingizini. Akaamka na kwenda chumbani kwa mama yake akaone kilichomkuta mama yake.

SASA TUNAENDELEA KUCHUKUA ODA KWA KITABU HIKI 👇. BADO WATU 47 TU IWE MWISHO WA KUCHUKUA ODA....WEKA ODA LEO IWE RAHISI KUKIPATA HIKI KITABU KWA BEI YA TSHS. 10000/= TU... 🙏.

Address

Africana
Dar Es Salaam

Telephone

+255785276697

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Fikra posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category