Miamia Trading Company

Miamia Trading Company We love trading and sharing of knowledge. Knowledge pertaining to trade. By sharing knowledge, we nurture skills and foster prosperity. And that is our motto.

Nurturing Skills, Fostering Prosperity. We are guided by the principle of "Prosperity for All." Sisi hufanya yale yanayotuvutia. Kazi yetu ni sehemu ya maisha yetu. Tunaamini kuwa ili tujivunie na tufurahie kile tukifanyacho ni sharti tukifanye kwa umaridadi. Tunaamini kuwa ili tufanye jambo kwa umaridadi ni lazima kwanza tulipende jambo hilo. Tunapenda kununua na kuuza. Tunapenda kushirikisha wen

gine katika ujuzi wa kununua na kuuza. Kwa kufanya hivyo basi Tunakuza Maarifa na Kuboresha Ustawi. Na hii ndio dhima yetu kuu. Kukuza Maarifa na Kuboresha Ustawi. Tunaongozwa na msingi wa "Ustawi kwa Wote".

09/09/2023
    inalipa au hailipi   ???
08/08/2023

inalipa au hailipi ???

Hatua 5 za
07/08/2023

Hatua 5 za

LET'S SEE HOW TO START A HEALTH COLLEGE IN TANZANIA===================1. Visit miamia.co.tz2. Write "health college" in ...
21/07/2023

LET'S SEE HOW TO START A HEALTH COLLEGE IN TANZANIA
===================
1. Visit miamia.co.tz
2. Write "health college" in the search bar
3. Click search and open the resulting page.

KARIBU KWENYE MIJADALA YA KIBIASHARA KWENYE CLUBHOUSEKwa wanaoijua clubhouse watakuwa wanaelewa kuwa ni sehemu sahihi za...
05/03/2023

KARIBU KWENYE MIJADALA YA KIBIASHARA KWENYE CLUBHOUSE

Kwa wanaoijua clubhouse watakuwa wanaelewa kuwa ni sehemu sahihi zaidi ya kujadiliana mana watu wanaweza kuongea na kusikilizana na kushauriana.

K**a hujaanza kutumia clubhouse na una smartphone basi download kupitia app store ana playstore. Ukishadownload jiunge kwa kutumia namba yako ya simu ama email. Ukimaliza rudi kwenye post hii na u click hii link hii:

https://www.clubhouse.com/c/join/fY3AoEGw

Utajiunga na kila panapokuwa na mada utaweza kushiriki. Mijadala itakuwa ya kiswahili. Ukikwama kujiunga tuma ujumbe whatsapp number +255748442442 usemao nimeshadownload clubhouse na nimejisajili ila nashindwa kujiunga na room ya Biashara Tanzania.

Kuanza, Kuendesha, Fursa za Biashara

UNABADILIJE MWAKA? MAMBO MAWILI YA KUFANYIA KAZI MWAKA 2022.------------------------------------------------JAMBO LA KWA...
02/01/2022

UNABADILIJE MWAKA? MAMBO MAWILI YA KUFANYIA KAZI MWAKA 2022.
------------------------------------------------

JAMBO LA KWANZA - KUTAFUTA MARAFIKI WAPYA

Rafiki mmoja wa thamani ni bora kuliko marafiki elfu wa hasara.

UKWELI NI KWAMBA

(i) Marafiki wa thamani ni wagumu sana kupatikana mana wanaangalia watanufaika na kipi toka kwako.

(ii) Marafiki wa hasara ni simple sana kuwapata mana wanakuwaga wapo wapo tu hawana mipango maalum ya kimaisha zaidi ya kuwa mizigo ama tegemezi kwa wengine.

(iii) Ili upate marafiki wa thamani lazima wewe mwenyewe uwe wa thamani. Jiulize una kipi cha thamani cha kumfanya mtu aamue kujenga urafiki nawewe. K**a huna basi endelea kusoma makala hii.

(iv) Unatakiwa kutemana na marafiki feki, wanafiki, wazushi na wasio na mipango ya kimaisha. Hawa watakulostisha tu.

(v) Huwa inachukua muda rafiki mpya wa thamani kukuamini, kukupenda na kukushirikisha kwenye mambo yake hivyo kuwa mvumilivu.

SASA UNAPATAJE MARAFIKI WAPYA WA THAMANI

(a) Tafuta magroup ya wanaojielewa na waliojikita kwenye mambo ya kimaendeleo mfano magroup ya biashara.

(b) Tafuta ujuzi na maarifa mapya ambayo yatakufanya nawewe uonekane wa maana kwenye magroup. K**a huna chochote ujuacho kwenye magroup kutakuwa kugumu sana.

(c) Pendelea kutoa ulichonacho ili nawe upewe ukitakacho. Mfano kuna mambo unayajua basi shea na wengine ili nao waone umuhimu wako. Usiwe mchoyo wa mambo mazuri. Kuna watu wakijua kitu ni siri yao hawawezi muelezea mwingine. Hahamu kuwa ukibania nawewe utabaniwa.

JAMBO LA PILI - KUONGEZA MAARIFA MAPYA

Jifunze mambo kadhaa mapya ili kujiongezea ujuzi.

(a) K**a upo kwenye biashara ama una ndoto za kufanya biashara basi jifunze mambo kadhaa yahusuyo matumizi ya mitandao ya kijamii kufanya biashara, utunzaji wa kumbukumbu za biashara, jinsi ya kutumia vyema vikoba kujikwamua kwenye biashara, mbinu za kukopa pesa benki, jinsi ya kujiwekea akiba, na kadhalika.

(b) K**a huna ndoto za kufanya biashara ila unataka kupiga mishe mishe tu basi jifunze matumizi ya mitandao ya kijamii kujenga jina na kuwasiliana na wapiga mishe wengine.

(c) Jifunze vitu vingine vinavyoongeza ujasiri na nguvu za mwili. Mfano wa yale unayoweza kujifunza yakakuongezea nguvu na ujasiri ni k**a kuogelea, kutazama movie za kutisha, na kadhalika.

(d) Jifunze skills nyengine ndogo ndogo kulingana na muda ulionao. Mfano wa skills nyengine ndogo ndogo ni k**a mitindo, mapambo, vipodozi, ubunifu, na kadhalika.

HITIMISHO
Nakutakia kila la heri katika kuuanza mwaka wako vyema na kwa mafanikio. K**a umependezwa na makala hii basi usiache kutembelea www.miamia.co.tz/swahili mara kwa mara. K**a una jambo la kuuliza bofya hapa ili upate sehemu ya kuulizia.

2022 hii hapa sasa. Biashara gani nzuri ya kufanya mwaka huu wa 2022?------------------------------------------------Ukw...
01/01/2022

2022 hii hapa sasa. Biashara gani nzuri ya kufanya mwaka huu wa 2022?
------------------------------------------------
Ukweli ni kwamba kila biashara ni nzuri na ina faida ndio maana unakuta biashara iliyomshinda mtu mmoja mwingine anaifanya na inamlipa.

Hivyo basi swala la kuwa biashara gani ni nzuri na yenye faida jibu lake ni kwamba biashara zote ni nzuri na zina faida.

JAMBO LA MSINGI NI HILI HAPA

Jambo la msingi ni kujua biashara gani ni nzuri kwako na biashara gani sio nzuri kwako. Hapa ndio panapotushinda wengi. Kuchagua biashara sahihi ni kazi ngumu sana.

Katika mambo mawili magumu kufanya maamuzi na kuchagua duniani la kwanza ni mpenzi sahihi na la pili ni biashara sahihi.

KUJUA K**A BIASHARA NI NZURI KWAKO

Unatakiwa kuangalia k**a hiyo biashara ipo kwenye orodha ya fursa zako. Kila mtu ana fursa zake. Ili fursa iwe yako lazima kuwe na mazingira wezeshi ya wewe kuiendesha biashara hiyo.

Mfano 1: Watu wawili wakiamua kulima. Wa kwanza akawa hana shamba, hana uzoefu, hana mtaji, hajui alime nini, na hajui soko lilipo. Mtu wa pili akawa ana shamba la urithi, amekulia kwenye mazingira ya kilimo alichokuwa anafanya baba yake, ana mtaji wa kulima, ana muda wa kutosha kusimamia shamba. Wa kwanza kilimo sio fursa yake. Wa pili ndio fursa yake.

Mfano 2: Mtu akiwa na gari la urithi akaamua kuligeuza gari hilo kuwa taxi na yeye akawa ndiyo dereva ukimlinganisha na yule mwenye gari la mkopo akampa dereva alete hesabu huku benki nao wakisubiri hesabu ya marejesho, yupi anaweza fanikiwa kwa haraka iwapo wote wana idadi sawa ya rasilimali nyenginezo?

TUNAZIJUAJE FURSA ZETU? HATUA TATU

HATUA YA KWANZA. Unatakiwa uanze kwa kuorodhesha rasilimali zote ulizonazo ikiwemo vitu, mali, fedha, maarifa, ujuzi, connection, muda, na kadhalika.

HATUA YA PILI. Ukimaliza kuorodhesha rasilimali ulizonazo orodhesha biashara zote unazoweza na ambazo unatamani kuzifanya.

HATUA YA TATU. Sasa linganisha rasilimali ulizonazo na biashara unazozitaka je ipi ambayo una rasilimali nyingi zaidi za kufanyia biashara hiyo? Utagundua kuna biashara unaweza kufanya kwa kutumia rasilimali ulizonazo. Anzia hapo na utafute vile ambavyo vinakosekana ili kufanya biashara hiyo.

HITIMISHO
Nakutakia kila la heri katika kuuanza mwaka wako vyema na kwa mafanikio. K**a umependezwa na makala hii basi usiache kutembelea https://www.miamia.co.tz/swahili mara kwa mara.

JE WAJUA MCHANGO WA BIASHARA NDOGO HUKO CHINA?---------------------------------------------------Zaidi ya nusu ya pato l...
07/12/2021

JE WAJUA MCHANGO WA BIASHARA NDOGO HUKO CHINA?
---------------------------------------------------
Zaidi ya nusu ya pato la taifa huko Uchina hutokana na biashara ndogo. Wamiliki wa biashara ndogo ndio wanaomiliki zaidi ya nusu ya hatimiliki za kibunifu huko Uchina. Biashara ndogo huajiri zaidi ya nusu ya wachina wote. Biashara ndogo zapaswa kuheshimiwa.

NJIA BORA ZAIDI YA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUUZA BIDHAA AMA HUDUMA YAKO---------------------------------------------...
13/05/2020

NJIA BORA ZAIDI YA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KUUZA BIDHAA AMA HUDUMA YAKO
----------------------------------------------------------------
1. Jenga idadi kubwa ya followers kwa kuandika na kupost vitu vyenye manufaa kwa jamii.

2. Andaa ukurasa maalum wenye bidhaa zako ama huduma zako na maelezo ya upatikanaji na faida zake kwa mtumiaji.

3. Tengeneza namna ya kuwalink followers wako waitembelee ule ukurasa maalum wenye bidhaa zako ama huduma zako. Hapa unaweza kuwa unaibua hisia kwenye makala zako kisha unawaelekeza watu watembelee ukurasa wako wenye huduma ama bidhaa zako.

4. Weka akilini kuwa watu hutaka kutatuliwa matatizo yao hawataki bidhaa wala huduma zako. Hivyo ili uuze lazima uweze kuonesha bidhaa ama huduma zako zinatatuaje matatizo waliyonayo.

UMEONA HUO MMEA ULIPOOTA? BASI HATA MAFANIKIO YAKO YAPO HIVYO. HAIJALISHI UPO KATIKATI YA MAWE, MIBA, WANAFIKI, WAZANDIK...
12/05/2020

UMEONA HUO MMEA ULIPOOTA? BASI HATA MAFANIKIO YAKO YAPO HIVYO. HAIJALISHI UPO KATIKATI YA MAWE, MIBA, WANAFIKI, WAZANDIKI, ETC
--------------------------------------------------------
Kuna factor mbili tu kwenye mlinganyo wa mafanikio yako. K**a mafanikio ni Z basi jitihada ni X na Imani ni Y. Kumbuka

Z = X + Y Mafanikio ni jitihada jumlisha imani.

Address

MIAMIA TRADING COMPANY
Arusha
36596

Opening Hours

Monday 08:00 - 18:00
Tuesday 08:00 - 18:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 18:00
Friday 08:00 - 18:00
Saturday 08:00 - 17:00

Telephone

+255748442442

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Miamia Trading Company posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Miamia Trading Company:

Share

Category