08/09/2021
MAZUNGUMZO
Simba : Hivi Mtani hao watu uliowabeba hawakuchoshi??
Yanga :. Umeanza kunifata fata nikianza mimi usilalamike
Simba : Kwenye hao watu mmemkumbuka Mzee Akilimali au umeweka kina GSM tuu
Yanga : Kwan wewe umemtambua nani hapa
Simba : Nimeona wengi ila Mwakalebela hamjamuweka
Yanga : Mwakalebela asingetosha hapa
Simba : Jumla hao watu wako wangap kwani??
Yanga : Unataka idadi ya watu wangu
Simba : Ndio Swahiba
Yanga : Nipe iyo sabuni niwaogeshe ndo utawaona
Simba : Ushaaanza ubwege
Yanga : Tena kuwa makini uyo Mo Sports kwa kushirikiana na Vunja Bei wanaweza kukukaba usiku
Simba : Mimi nimejaza wadhamin wanatoa hela wewe umejaza wapigania Uhuru
Yanga : Halafu iyo sabuni hapo ikinyeshewa Mvua si inayeyuka?
Simba : Nikuuulize wewe unaechunguza mambo ya watu
Yanga : Halafu Swahiba mbona hawajakufanyia uzinduzi
Simba : Hilo hata mimi limeniuma
Yanga : Hawakupendi, wanaona hauna hadhi ya kufanyiwa sherehe Serena
Simba : Acha uchonganishi wewe
Yanga : Halafu Majina ya Wachezaji mtaweka kiunoni??
Simba : Kwann
Yanga : ile sehemu ya jina si mmeweka Sabuni ya Boss
Simba : Unaona wivu eeh na wewe kaweke godoro la Boss wako Mgongoni
Yanga : Halafu Majina niweke kwenye Bukta??
Simba : Utajua Mwenyewe
Simba : Halafu Mtani mbona hujatengeneza Jezi za watu Wanene
Yanga : Yanga hatuna wanene
Simba : Na jezi za watoto je?? Au hakuna Watoto wa Yanga
Yanga : (Kimoyomoyo) Hapa kaniweza, 🤔 Watavaa wakiwa wakubwa
Simba : Jezi za Wanawake nazo mbona hamna
Yanga : Kaka unauliza maswali mengi sana hebu hangaika na yako
Yanga : Halafu nasikia iyo nembo ikipigwa na upepo inabanduka
Simba : Endelea kusikia
Yanga : Basi tusitumie nguvu kubishana Tusubir kuona mwisho wa Msimu jezi ya nani itakua imepauka
Simba : Sawa Tusubir pia tuone jezi ya nani itabeba Kombe
Yanga : 😏😏