Monjes HOTEL

Monjes HOTEL KARIBUN KWA HUDUMA SAFI YA MALAZI NA VINYWAJI

*** LOVE STORY ***Ilikuwa k**a saa nne usiku ambapo John alipigiwa simu na dada mrembo ,ambae anampenda kwa moyo wake wo...
21/10/2015

*** LOVE STORY ***

Ilikuwa k**a saa nne usiku ambapo John alipigiwa simu na dada mrembo ,ambae anampenda kwa moyo wake wote lakini kila akijaribu kumueleza hisia zake binti mrembo hamwelewi, John alipopokea cm akasikia sauti taaam ikisema:
“Ombi lako nimelikubali naomba uje nyumbani kwani niko peke yangu nahisi ndo chance pekee ya mimi na wewe kukutana na kuongea yetu zaidi", mrembo alimaliza kuongea ,

Bila kupoteza muda John akafika kwa binti, alipoingia akakaribishwa mpaka chumbani, kwakuwa jiji la Dar lina joto binti alikuwa amevaa khanga moja tu laini sana iliyoweza ipa nafasi lenzi ya jicho la John kuona mpaka ndani...

*** Sorry jamani battery low siwezi kumalizia sijui nifanyeje!?
Au tufanye tu "Wamedondokewa na Nyumba wamekufa wote!, na Story imeisha...!!......
picha haihusikiiiiiiii......

HABARI ILIYOTUFIKIA PUNDE...HATIMAYE MAMA IZENGO HOTEL YAPATA MKUU WA IDARA YA ULINZI
13/06/2015

HABARI ILIYOTUFIKIA PUNDE...

HATIMAYE MAMA IZENGO HOTEL YAPATA MKUU WA IDARA YA ULINZI

22/08/2014

DOMINIKA YA 21: MATHAYO 16:13-20

Injili ya dominika hii inahiridhisha matunda imani juu ya Kristu. Lakini pia inaonyesha ni kwa jinsi gani imani ituokoayo inavyotufikia. Kristu alitenda ishara na miujiza mikubwa, lakini watu bado hawakumtambua. Hivyo anapenda kufahamu wanaisrael wanamtambuaje. Wakiwa gizani bado wanamwona Kristu k**a mmoja wa manabii (Mathayo 16:14). Ndipo anapowageukia wanafunzi wake na kuwauliza "Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?" (Mathayo 16:14). Petro,msemaji mkuu kati ya wale Mitume anatoa jibu ambalo linabadilisha maisha yake na nafasi yake katika Kanisa. Kutokana na hilo jibu Kristu anambadili jina Simoni, anamwita "…..Wewe ndiwe Petro" (Mathayo 16:18) yaani “Petros” (kwa kiswahili Mwamba) kwa lugha ya kigiriki iliyotumika kuandika Biblia. Tunafahamu kupitia maandiko matakatifu kuwa katika kubadili majina ya watu wake (Abram kuwa Abraham ama Sauli kuwa Paulo n.k), Mungu anatengeneza safari mpya, ama nafasi mpya ndani ya watu hao. Hivyo Simoni wa zamani anakua mpya katika jina “Petro”.

Kwanini basi abadilishwe jina? Anapewa kazi gani mpya huyu Petro?

Kujibu swali hili, ni vyema turejee katika Agano la Kale katika somo la kwanza la dominika hii. Humu tunapata fundisho kubwa. Tunakutana na mtumishi wa Mungu aitwaye “Eliakimu”. Huyu alifanywa na Mungu kuwa “Waziri Mkuu” kipindi cha Mfalme Hezekia. Lakini alipewa nafasi ya pekee sana maana Mungu alisema "...nitamwita mtumishi wangu Eliakimu...nitamkabidhi yeye mamlaka...naye atakua baba kwa wenyeji wa Yerusalemu, na kwa nyumba ya Yuda (Isaya 22:20-21). Japo Yerusalemu ilikuwa na Mfalme wake Hezekia, tunaona huyu Eliakimu akipewa mamlaka ya kuangalia na kusimamia shughuli za ufalme wote wa Hezekia. Lakini maneno ya ziada ya Mungu juu yake Eliakimu yanatushangaza zaidi maana Eliakimu anapewa “ufunguo” wa nyumba ya Daudi (Isaya 22:22). Kwa ufunguo huo, katika nyumba ya Daudi, Mungu anasema "...yeye atafungua wala hapana atakayefunga, naye atafunga wala hapana atakayefungua........naye atakua kiti cha utukufu kwa nyumba ya baba yake (isaya 22:22-23). Ni vyema kukumbuka kuwa pamoja na mamlaka yote haya, bado Eliakimu yu chini ya mfalme Hezekia. Maneno hayo aliyasema Mungu mwenyewe. Vile vile katika Injili, tunaona Mungu (Mwana) anarudia maneno yale yale kwa mwamba Petro. Mungu anatengeneza mamlaka ya “waziri mkuu kwa Petro” katika Yerusalemu mpya ambayo ni Kanisa. Anamwambia Petro.."Nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni" (Mathayo 16:19). Hayo aliyesema baada ya kusema kuwa atalijenga Kanisa lake juu ya mwamba Petro (Mathayo 16:18) na sifa kuu ya Kanisa hilo ni kuwa kamwe haliwezi kukumbwa na upotofu wa imani. Ndio maana kamili ya maneno "milango ya kuzimu haitalishinda" (Mathayo 16:18). Kwa ufupi ni kuwa Petro anapewa ahadi ya kufanywa “Papa” yaani baba mtakatifu mwenye "kiti cha utukufu (Isaya 22:23).K**a nafasi ya Papa ndiyo hiyo ya waziri mkuu, bila shaka katika nafasi ya mfalme Hezekia, anasimama Kristu mwenyewe. Mfalme ndiye ambaye waziri mkuu mamlaka ya kufunga na kufungua. Kanisa, japo lilianza rasmi siku ya Pentekoste, tayari Askofu Mkuu na mkubwa wa Kanisa hapa duniani alichaguliwa na Mungu mwenyewe na sifa na mamlaka ya uongozi wake yakawekwa bayana.

Ikawaje Petro kupewa nafasi hiyo ya pekee?

Turejee jibu alilotoa Petro juu ya ukweli kuhusu Kristo. Anasema "...wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliyehai (Mathayo 16:16). Anaonyesha imani ya ajabu. Lakini dominika zilizopita tumeona kuwa imani si jambo alipatalo binadamu kwa nguvu zake mwenyewe. Hii ni zawadi aitoayo Mungu (Waefeso 2:8). Ndipo anapokumbushwa Petro kuwa .." mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni " (Mathayo 16:17). Hivyo Mungu k**a Mfalme, japo anao mawaziri wake wakuu yaani Mapapa katika umoja wa Maaskofu, ndiye haswa mwenye Kanisa. Analipa imani Katoliki na ndiye anayewafanya Maaskofu na Mapapa wasiweze kamwe kupotosha imani, maana si miili na damu zao, bali ni Mungu mwenyewe aliye mbinguni. K**a ni Mungu alifunuliaye Kanisa ukweli juu ya imani, iweje basi tuweke hofu juu ya yale Kanisa linayotufundisha? Iweje tushindwe kujongea kupokea Sakramenti za Kanisa haswa zile za Kitubio na Ekaristi? Si Baba Mtakatifu na Maaskofu katika “mwili na damu” walioamuru haya, bali ni Mungu Baba aliye mbinguni.
SIKU NJEMA

15/08/2014

SOLEMNITY OF THE ASSUMPTION OF MARY : KUPALIZWA KWA MAMA MARIA MBINGUNI - 15 AGOSTI 2014

“Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili” (Ufunuo wa Yohana 12:1)

Toka karne ya 4 Kanisa limekua likikumbuka “kulala” yaani Dormition, na baada ya kulala “kupalizwa” mbinguni (Assumption) kwa Mama Maria. Katika kuleta msisitizo wa umuhimu wake, Kanisa likasimamia zaidi katika “kupalizwa” kwake. Kwanini? Hii tutaona zaidi hapo baade. Leo hii na kila mwaka, tarehe 15 Agosti Kanisa linaadhimisha sikukuu hii ya “Imani ya Mitume” isiyopingika. Sio kwa uwezo wake mwenyewe, bali haswa kwa neema za Mungu, Kanisa linakiri kuwa Mama Maria alipalizwa mbinguni “mwili na roho”.

Kwa neema za Mungu, amefanywa Mtakatifu mkuu kuliko wengine wote. Mpaka itakapofika mwisho wa dunia hii (siku ya hukumu), Watakatifu wa Mungu walio mbinguni, humwona Mungu wakiwa katika hali ya roho tu (maana roho yaani “soul” kamwe haifi binadamu apatapo mauti. Mwili huoza, lakini roho hupokelewa na Mungu (k**a roho imetenda mema) ama hupokelewa na kuteswa na shetani kutokana na dhambi za mtu huyo na roho yake) . Hivyo Watakatifu wa mbinguni yawapasa kusubiri ufufuko wa miili yao siku ya mwisho ndipo wawe na ukamilifu wa binadamu (mwili kuungana tena na roho) ambayo ndiyo zawadi ya matendo yao mema. Hivi si k**a ilivyo kwa Mama Maria. Yeye yu mbinguni k**a binadamu kamili katika mwili na roho. Baada ya kumaliza kipindi chake mbinguni, yaani kifo chake (maana Mababa wa Kanisa na Wanateolojia wanaamini kuwa Mama Maria alikufa kifo cha kawaida cha binadamu ili kushiriki pia mateso ya Kristu kabla ya kushiriki utukufu wake baada ya kifo), hivyo punde baada ya “kulala” (Dormition), roho yake ikapokelewa na Kristu lakini pia mwili wake ukafufuliwa na kupalizwa na Kristu ili awe kamili katika ufalme wa mbingu. Hivyo Mama wa Mungu (Maria), pamoja na Kristu (Mungu Mwana) wanaishi katika hali zote mwili na roho mbinguni.

TUNAPATA WAPI FUNDISHO HILI LA IMANI?

Mapokeo ya Mitume (Apostolic Tradition) yanatufundisha imani hii lakini pia yakiambatanishwa na Biblia k**a kitabu kitakatifu. Rejea maandiko ya hapo juu yanayotolewa katika kitabu cha Ufunuo kilichoandikwa na Mtume Yohane kabla ya kifo chake. Mtume Yohane anapata ufunuo, anaona hekalu la Mungu lililoko mbinguni (Ufunuo wa Yohana 11:19), ndani mwa hekalu hilo analiona “sanduku la agano”. Kanisa na Watakatifu toka karne ya 2 wamemtafsiri Mama Maria k**a sanduku jipya la agano. Jinsi lile sanduku la zamani lilivokua safi bila doa, likibeba “mana” na amri kumi za Mungu (Waebrania 9:4) na jinsi Mungu alivyopenda kukaa humo pasafi (Kutoka 25:8) ndivyo hivyo hivyo Mungu alipoamua kuchagua sanduku jipya katika Maria ili aweze kukaa k**a “mana” ya kweli, kukaa k**a “amri mpya (Neno)” na mwisho kukaa k**a “Mungu” katika sanduku Maria. Mfano huo ni ukweli tosha kabisa ndio maana Injili ya Luka kwa makusudi kabisa inafanya mfanano kati ya sanduku la zamani na sanduku jipya (Luka 1: 39-45). Matokeo muhimu yaliyonakiriwa katika kitabu cha 2 Samweli 6:1-11 juu ya sanduku la agano la zamani ndiyo yanajitokeza tena kwa Maria. Kwanza sanduku linasafirishwa mpaka “mji mmoja wa Yudea” (2 Samweli 6:1-11), vivyo hivyo Maria baada ya kupata habari juu ya mimba ya Elizabeth, anasafiri mpaka “mji mmoja wa Yudea” (Luka 1:39). Mfalme Daudi katika kuliona sanduku la agano la zamani anacheza kwa furaha mbele ya sanduku hilo (2 Samweli 6:14). Vivyo hivyo mtoto Yohana Mbatizaji anaruka kwa furaha tumboni mwa mamaye Elizabeth baada ya kusikia sauti ya Maria (Luka 1:41). Tunaona pia mfanano wa sentensi zenye mshangao mkubwa wazitoazo Daudi na Elizabeth juu ya ugeni huo wa sanduku hizo mbili mpya na zamani. Daudi analipokea sanduku kwa kusema “....Litanijiaje (mimi) sanduku la Bwana? (2 Samweli 6:9), kwa upande wake Elizabeth anapomwona Maria anasema “Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?” (Luka 1:43). Mwisho kabisa tunaona kuwa idadi ya miezi ya ugeni wa sanduku hizo mbili huko Yudea ni sawa. Katika amri ya mfalme Daudi, Sanduku la kale likakaa nyumbani kwa Obed-edomu kwa miezi mitatu (2 Samweli 6:11). Tunaona pia kuwa Luka anatuambia Maria alikaa na Elizabeth kwa miezi mitatu pia (Luka 1:56)

Hivyo hatuna shaka kuwa Mama Maria ni sanduku jipya la agano. Haya yameandikwa na kusemwa pia na Mababa wa Kanisa, Watakatifu wa Mungu karne ya 2-4 za mwanzo (Mt. Hippolytus 170-236, Mt. Ephrem 306-373, Mt. Cyril 315-387, Mt. Athanasius 296-373, Mt. Gregory Thaumaturgus 213-270, Mt. Ambrose 339-397, Mt. Jerome 345-420 na wengine watakatifu wengi). Ndipo Kanisa na Watakatifu hawa wanavyosoma na kutafsiri maandiko katika kitabu cha ufunuo wa Yohana.

Kitabu cha ufunuo kinasema “Kisha Hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana ndani ya hekalu lake. (ufunuo wa Yohana 11:19). Punde tu baada ya kusema hayo, Yohana anaongelea maono mapya juu ya mwanamke aliyevikwa taji la jua na kichwa chake kina nyota 12. Anasema ...” Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili (Ufunuo wa Yohana 12:1). Akiendelea kuelezea ufunuo huo, ni wazi kabisa Mama Maria (Sanduku jipya la agano) anaongelewa akiwa Malkia wa mbingu aliyefanywa na Mungu kuwa mkuu kuliko watakatifu wote kuliko hata malaika wote. Pia anaelezea jinsi Joka kubwa (shetani na malaika wake waovu) linavo jongea likipenda kumnyang’anya Mama mtoto anayekaribia kuzaliwa. Lakini mtoto huyu ndiye “atakayewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi (Ufunuo wa Yohana 12:5). Mtoto huyu ni Yesu Kristo, Mwana wa Maria.

SIKUKUU HII INA UMUHIMU GANI KWETU?

Katika kusheherekea sikukuu ya kupalizwa mbinguni Mama Maria, Kanisa linataka kutukumbusha vitu vikuu viwili:

1. Kwamba jinsi Mama Maria alivopalizwa mbinguni mwili na roho (assumption), ndivyo hivyo nasi tutakavyo palizwa siku ya mwisho. Roho zetu zinazopokelewa na Bwana siku ya mauti zitapata nafasi ya kukutana tena na miili yetu itakayofufuliwa. Nasi tutakua binadamu kamili nyumbani kwa Baba k**a ilivyo sasa kwa Maria. Hivyo sikukuu hii inatupa Tumaini kubwa mno kuwa Mungu ndiye muweza na hatatuacha miili yetu kuoza ardhini. Atatufufua siku ya mwisho

2. Pia Kanisa linatukumbusha umuhimu wa kumkimbilia Mama Maria katika maombezi yake kwetu. Maombezi yake ndiyo yenye matunda zaidi kuliko ya watakatifu wengine. Yeye huomba daima katika mapenzi ya Mungu. Hanyimwi lolote aombalo kwa Mwanaye. Tumkimbilie huyu Mama atulete karibu na Mungu tupate msamaha wa Mungu. Ndiyo maana katika historia ya Kanisa, Mama Maria amekua akiwatokea watu mbalimbali akiihasa dunia nzima kumfuata Kristu, kutubu na kutomkasirisha Mungu. Katika hali ya mwili na roho amewatokea watu huko Fatima, Lourdes Ufaransa, Guadalupe, Laus, Knock e.t.c

MAMA MARIA ULIYEPALIZWA MBINGUNI, UTUOMBEE SASA NA SAA YA KUFA KWETU

DOMINIKA YA 18: THE MULTIPLICATION OF LOAVES: KRISTU ANALISHA WATU ZAIDI YA 5,000: MATHAYO 14:13-21Injili ya wiki hii in...
31/07/2014

DOMINIKA YA 18: THE MULTIPLICATION OF LOAVES: KRISTU ANALISHA WATU ZAIDI YA 5,000: MATHAYO 14:13-21

Injili ya wiki hii inaelezea ukuu na utukufu wa Kristu pale anapolisha umati wa watu usiopungua elfu tano (5,000). Japo Kristu anahiridhisha ukuu wake kwetu kwa maajabu haya, tunashawishika kwa haraka sana kutafakari na kufurahia tu maajabu afanyayo huku tukikosa nafasi ya pekee kutafakari pia mengine yanayoonekana kumezwa na utukufu huo aliodhihirisha. Utukufu na uweza ni moja kati sifa za Kristu lakini kubwa kuliko zote ni huruma yake.

Tukio hili la kulisha umati wa watu 5,000 (Mathayo 14:13-21) lilitanguliwa na kifo cha Yohane Mbatizaji aliyeuawa kwa kukatwa kichwa na Herode (Mathayo 14:10). Kristu alipopata habari hizo, Injili inatuambia kuwa “…..aliondoka…..akaenda mahali pasipo na watu, faraghani. (Mathayo 14:13). Twaweza jiuliza, ni kwanini akapenda kujitenga? Mahali pengi katika Biblia Kristu aliona umuhimu wa kuwa peke yake na kupeleka maombi yake kwa Baba. Mara nyingi anawaacha wanafunzi wake anatafuta muda wa pekee akiomba. Kuna siri kubwa katika tendo hili ndio maana anatuhimiza kuwa “…..usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele ya Baba yako aliye sirini” (Mathayo 6:6). Ni wazi Kristu hakupendezwa na alisikitishwa mno na kifo cha Yohane. Akahitaji kujificha na kuongea na Baba “..aliye sirini”. Mungu huyu Mwana, anayo huruma ya ajabu na huwa karibu nasi katika hali ya majonzi. Mfano ni jinsi alivyomlilia rafikiye Larazo (Yohane 11:35), pia alivyoililia Yerusalemu katika hali yao ya kutokubali wokovu wake (Luka 19:41).

Akiwa katika hali hiyo ya maongezi na Baba, anaambiwa kuwa umati mkubwa wa watu umemfuata huko aliko. Watu hawa wametoka mbali lakini Kristu yu katika maombi. Tutafakari kwa ndani jambo alilofanya Kristu. Alipowaona, Mtume Mathayo anatuambia kuwa Kristu “….akawahurumia…(Mathayo 14:14). Tujiulize, Je ni mara ngapi tunapokua katika maombi ya shida zetu hatupendi kusumbuliwa na shida za wengine? Tuko tayari kusitisha maombi kwa muda na “….kumpenda jirani yako k**a unavyojipenda mwenyewe…”? (Marko 12:31). Lakini hapa Kristu …”akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia” (Mathayo 14:14). Tena akafanya zaidi ya kuwahurumia….”akawaponya magonjwa yao” (Mathayo 14:14). Mwisho kabisa hata baada ya kuwalisha chakula na ….”alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba (Mathayo 14:23)

Sifa kuu ya Kristu ni huruma. Ndiyo huruma hiyo hiyo inayokuja kufanya maajabu makuu tunayopenda sana kutafakari na kuyaona k**a binadamu. Ni vyema zaidi kutafakari huruma yake kuliko. Huruma hiyo ikamfanya alishe umati wa watu zaidi ya 5,000 maana Injili inatuambia hao elfu tano ni bila kuhesabu “..wanawake na watoto” (Mathayo 14:21). Watu wakala na “kushiba” na baada ya kushuhudia mwujiza wakasema “….hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni (Yohane 6:14). Wakiwa bado gizani (yaani hawajui kwanini Kristu amekuja duniani), wanataka “…kumshika ili wamfanye mfalme” (Mathayo 14:15). Lakini Kristu akapenda kuendelea na maombi yake kwa Baba hivyo……”akajitenga, akaenda tena mlimani yeye peke yake (Mathayo 14:15).

Basi Biblia inatuambia kuwa Kristu “……..aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai siku zote ili awaombee (Wahebrania 7:25). Anafanya maombi yasiyoisha milele huko mbinguni, lakini pia anaona umati wa watu wake Duniani tukimfuata. Jinsi alivyoonyesha huruma kwa wale zaidi ya 5,000 ndivyo anavyotuonea huruma nasi. Je, uko tayari kupeleka shida zako kwake? Unayo magonjwa ya dhambi anayoweza kuyaponya? Je, unayo njaa ili nawe ule ushibe? Basi anakualika siku ya Jumapili hii maana k**a wale 5,000 ameandaa chakula (Ekaristi) kwa wote wenye njaa. Wapate kushiba na kubeba hata masalio. Unapomla “unatosheka” na kwa kuwa hatuwezi kumaliza mwili wake, salio bado ni Yeye mwenyewe na tunapeleka salio hilo kwa wengine ili wapate kumfahamu pia washibishwe.

RUKSA KUISAMBAZA ILI WATU WA MUNGU WAPATE INJILI

26/07/2014

Dominika ya 17 ya Mwaka July 27, 2014

Tafakari ya somo la Injili kutoka Matayo 13:44-52

UFALME WA MBINGUNI “HAZINA ILIYOFICHWA”

Katika injili ya leo tunafundishwa kuwa ufalme wa mbinguni haupatikani kirahisi ila umefichwa na ya kuwa watakao kuingia lazima wafanye mang’amuzi ya dhati kuutafuta au kwa maana nyingine waanze safari ya kuutafuta.

Ikiwa umesoma kwa uangalifu maneno ya Mungu katika injili ya leo utagundua kuwa imetupasa kwanza “kuamua” kisha kuanza “kuutafuta” na tukiisha kuupata ndipo tunapata furaha ya kweli. Injili inaweka wazi kwamba safari ya kuingia Ufalme wa mbinguni inaanzia hapa duniani na ndiyo maana tunaanza kuonja furaha ya ufalme wa Mungu hapa duniani ikiwa tumeacha vyote na kuanza kuutafuta. “Yesu akajibu, “Ninawaambieni hakika, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, kaka, dada, mama, baba, watoto au shamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya kuitangaza Habari Njema, ambaye hatalipwa katika ulimwengu huu mara mia zaidi: nyumba, kaka, dada, mama, watoto, mashamba na mateso pia; na kupewa uzima wa milele katika ulimwengu ujao Marko 10:29-30”. Kulingana na maneno haya ya Yesu katika safari ya kuanza kuutafuta ufalme wa Mungu lazima kuna swala la “kuacha” kuacha maana yake ndiyo kuingia gharama ya kujinyima na kujitenga na mambo ya ulimwengu ili kumtumikia Mungu kila siku na kisha tutaupata mema ya Mungu hapa duniani lakini zaidi sana kuipata hiyo Ahadi ya kuingia katika Ufalme wa mwana wa pendo lake.

Yesu anatumia mifano kuwafundisha wanafunzi wake juu ya ufalme wa Mungu kwa jinsi ya kipekee kwa kufananisha na kitu cha thamani, na mifano aliyoitumia hapa ni “hazina”,” lulu” na “samaki wazuri” ambapo vyote ni mifano ya vitu vya thamani kwa sura za kidunia; pia ikumbukwe kuwa hapa katika mfano wa samaki, wale samaki wazuri huchaguliwa na kutunzwa lakini wabaya kutupwa; Lakini kutupwa kwetu sisi hakutakuwa k**a kutupwa kwa samaki sisi tutatupwa kwenye tanuru la moto wa milele rejea “Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. Na watawatupa hao waovu katika tanuru ya moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno Matayo 13:49-50”.

Kwa upande mwingine hazina inayozungumziwa hapa ni mfano wa fedha au dhahabu ambapo wewe utakuwa shahidi kuwa iwapo utahakikishiwa kuwa katika shamba fulani mna dhahabu au almasi basi utafanya jitihada zote kulinunua. Au ukisikia kuna kazi fulani hata k**a ni ngumu lakini ina ujira mkubwa utajitutumua kwa vyovyote ili uifanye na kisha upate hiyo hazina. Yesu anatumia mfano wa “kuuza vyote” ili kuupata ufalme wa Mungu. Hapa anajaribu kutusaidia kubadili namna yetu ya kuthamini pasipo kubadili namna yetu ya kuthamini vitu hatutaweza kuupata ufalme wa mbinguni. Hatua ya kwanza kabisa mtu anapoanza kuutafuta Uflame wa mbinguni ni kuwa na kitu kinachoitwa “badiliko la thamani” (Change of value) yaani kutambua kuwa hakuna kitu cha thamani au cha muhimu k**a Ufalme wa mbinguni, k**a Mtakatifu Paulo alivyowahi kusema “Kwa hiyo, kwa kweli naviona vitu vyote kuwa hasara kwa sababu ya thamani bora zaidi ya kumjua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa sababu yake nimekubali hasara ya vitu vyote nami naviona kuwa takataka nyingi ili niweze kumpata Kristo Wafilipi 3:8”. Kwa bahati mbaya hazina hii ya Ufalme wa mbinguni imefichwa ili yeyetu aliyehamua na yu tayari kuutafuta ndiye atakayeupata. Wengi tunafahamu jinsi ambavyo watafuta vito vya thamani k**a vile dhahabu au almasi huthubutu hata kuzama migodini bila kujali hatari zilizopo ili tuu wakipate kitu cha thamani “hazina”. Hata wewe mwenyewe ni shahidi wa maisha yako, utagundua kuwa wakati mwingine upo radhi usiende kanisani siku ya dominika au kujitoa katika utume mbalimbali kwa namna fulani kisa tuu uweze kuwahi katika kazi zako za kujiongezea kipato (kitu cha thamani). Hii ni namna ya jinsi unavyotoa kipaumbele kupata hazina za hapa duniani ungawa sote twajia hazifai kitu. “Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba. Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba. Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako Matayo 6:19-12” K**a hazina yako umeiwekeza kuupata Ufalme wa mbinguni basi hata hazina/mali zako utazitumia kuujenga ufalme wa Mungu. Na ndiyo maana halisi ya neno “hazina yako ilipo ndipo na moyo wako ulipo. Lakina k**a moyo/hazina wako upo katika hazina za hapa duniani na unatatumia nguvu zako kujitaabisha kupata mali/hazina za duniani kamwe hautaupata Ufalme wa mbinguni ” Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa mbinguni na haki yake, na haya yote mtaongezewa Matayo 6:33. Haimaanishi kwamba tusijishughulishe hapa duniani, la; kwanza Ufalme wa mbingu kisha mengine kwa ziada.

Hivyo, injili ya leo inatukumbusha kuacha vyote kwa ajili ya kuupata Ufalme wa mbinguni na ya kuwa wawezao kuupata Ufalme ndio hao wautafutao tena kwa bidii,. Imetupasa pia kukiri kuwa Ufalme wa Mbinguni unastahili majotoleo hayo kwani hakuna jambo jingine la muhimu kwa maisha ya binadamu hapa duniani zaidi ya kumjua Mungu, kumtumikia na mwisho kupokelewa katika ufalme wake mbinguni. Mtu aliyetayari kuacha yote kwa ajili ya Ufalme basi yu tayari kuacha dhambi na kuzichukia, kujitenga na ulimwenngu na anasa zake, ndiye aliyetayari kuwasaidia na wengine wamjue Mungu; Aliyetayari kutoa uhai wake (muda wake, chakula chake nk.) kwa ajili ya wengine na pia kuwa kuwa jasiri wa kuifia imani yake katika Kristu Yesu.
Hivyo basi na tumwombe Mungu atujalie hekima ya kuchagua mema k**a alivyoomba mfalme Solomoni ili hekima hiyo itufae hapa duniani na kutusaidia kuchagua na kufuata njia nzuri iletayo uzima na ielekeayo kwenye Ufalme wa mbinguni, pia tuombee familia zetu na familia zote duniani na hasa tuwaombee wazazi na viongozi waweza kuwachagulia na kuwarithisha watoto hekima hii ya kumchagua Mungu na kutoa kipaumbele kwa Ufalme wake kuliko jambo jingine lolote hapa duniani. Tudumu katika sala na tutake sana kufuata mambo ya uzima ule ujao na kutaka sana kumjua Mungu ili tuwe na amani yake imetimizwa ndani yetu.

Tumsifu Yesu Kristo

28/06/2014

KUTOKANA NA MAOMBI YENU NIMEONA NIWAPE RATIABA YA HATUA HII YA MTOANO 16 BORA

Jun 28, 2014
Brazil
V.
Chile
1:00 usiku

Colombia
v.
Uruguay
5:00 usiku

Jun 29, 2014
Netherlands
v.
Mexico
1:00 usiku

Costa Rica
v.
Greece
5:00 usiku

Jun 30, 2014

France
v.
Nigeria
1:00 usiku

Germany
v.
Algeria
5:00 usiku

Jul 1, 2014

Argentina
v.
Switzerland
1:00 usiku

Belgium
v.
United States
5:00 usiku

AHSANTENI SANA

27/06/2014

KESHO JMOSS TRH 28.6.2014 TUNAWALETEA:-

BRAZIL
V.
CHILE
1:00 USIKU

COLOMBIA
V.
URUGUAY
5:00 USIKU

KARIBUNI NYOTE MAMA IZENGO HOTEL

25/06/2014

LEO TRH 25.6.2014 TUNAKULETEA:-

Nigeria
V.
Argentina
1:00 USIKU

Bosnia-Herzegovina
V.
Iran
1:00 USIKU

Honduras
V.
Switzerland
5:00 USIKU

Ecuador
V.
France
5:00 USIKU

KARIBUNI PIA USISAHAU KULIKE MAMA IZENGO HOTEL

VINYWAJI  PIA  VIPO  UTAKUNYWA  KWA  STAILI  YAKO  UNAYOIPENDA
15/04/2014

VINYWAJI PIA VIPO UTAKUNYWA KWA STAILI YAKO UNAYOIPENDA

Address

Babati
Manyara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Monjes HOTEL posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share