03/09/2018
WAOMBEENI WANAOWAUDHI.
Amri za Kristo ni sehemu muhimu sana katika Ushirika wetu. Tusipojaribu kuziweka katika mawazo yetu, na kuzifuata, hatuna sehemu katika Mwili wa Kristo. " Matendo " ya " imani " yetu yanadhihirishwa k**a ni hai au yamekufa. Hebu natuyatafakari kila mara, na yawe msingi wa matendo yetu yote.
1. Wapende adui zako; watendee mema wakuchukiao.
" ... lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi;... " (Mathayo 5:44).
2. Usiwapinge waovu: mtu akikupiga shavu la kushoto, mpe na la kulia.
" ...lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili. Na mtu atakaye kukush*taki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia " (Mathayo 5:39, 40).
3. Usilipize kisasi: epukana na hasira: kubali kupata hasara.
" K**a yamkini, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote. Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana, imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana " (Warumi 12:18, 19).
4. Mtu akichukua mali yako, usiulize urudishiwe.
" Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang' anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu. Mpe kila akuombaye, na akunyang' anyaye vitu vyako, usitake akurudishie " (Luka 6:29, 30).
5. Patana na adui wako upesi, hata kukubali makosa kwa ajili ya amani.
" Patana na msh*taki wako upesi, wakati uwapo pamoja naye njiani; yule msh*taki asije akakupeleka kwa kadhi, na kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani " (Mathayo 5:25).
" Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnash*takiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang' anywa mali zenu " (1 Wakorintho 6:7).
6. Usisumbukie utajiri: kuwa tayari kutenda mema, wape wakuulizao: wasaidie wahitaji
" ...ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo " (1 Timotheo 6:8).
" ...kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni, mkijitahidi "
(Warumi 12:13).
" Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka k**a hizi ndizo zimpendezazo Mungu " (Waebrania 13:16).
" Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli