Muvi Na Burudani

Muvi Na Burudani Ijue muvi unayotaka kuangalia. Makala za wasanii na waigizaji.

Vichupa vipya mwezi huu.
05/03/2025

Vichupa vipya mwezi huu.

Siku ya leo mastaa mbali mbali wanaadhimisha siku zao za kuzaliwa na k**a wewe ni mmoja wapo basi nikutakie kheri ya sik...
24/02/2025

Siku ya leo mastaa mbali mbali wanaadhimisha siku zao za kuzaliwa na k**a wewe ni mmoja wapo basi nikutakie kheri ya siku yako ya kuzaliwa!

Miongoni mwa waigizaji hao ni pamoja na mkongwe Dominic Chianese anaeadhimisha miaka takribani miaka 93 tangu alipozaliwa mnamo trh 24 february 1931 huko New York City, U.S. Mwamba amehusika kwenye filamu nyingi sana series na vipindi mbalimbali kwenye tv.

Dominic Chianese ameigiza katika filamu na vipindi vya televisheni zaidi ya 50, maarufu zaidi akiwa k**a Uncle Junior kwenye The Sopranos. Uwepo wake katika tasnia ya filamu na televisheni umeanzia miaka ya 1970 na amekuwa sehemu ya filamu za kihistoria k**a The Godfather: Part II (1974) na Dog Day Afternoon (1975).

Mbali na filamu, ameonekana pia kwenye vipindi vya televisheni maarufu k**a Boardwalk Empire, The Good Wife, Law & Order, na Blue Bloods. Kando na uigizaji, Chianese pia ni mwimbaji na amekuwa akitumbuiza kwa nyimbo za Italia na mziki kwa ujumla wake.
Maisha yake yanaakisi safari ya msanii aliyejitoa kwa sanaa kwa miongo kadhaa, na mchango wake katika filamu na televisheni umeacha alama isiyofutika. Katika umri wa zaidi ya miaka 90, anaendelea kuwa sehemu muhimu ya historia ya burudani.

Filamu gani ya Dominic Chianese unayoikubali?

Liam Neeson mwanajeshi wa zamani wa Marekani aliyetumikia jeshi kwa uadilifu na ufanisi mkubwa  anageuka kuwa  mwizi maa...
24/02/2025

Liam Neeson mwanajeshi wa zamani wa Marekani aliyetumikia jeshi kwa uadilifu na ufanisi mkubwa anageuka kuwa mwizi maarufu lakini mwenye busara za kipekee. Anafanikiwa kuiba kiasi kikubwa sana Cha fedha lkn Cha kushangaza ni namna alivyozihifadhi bila kuzitumia Katika harakati zake anakutana na mrembo Annie na kuanzisha nae uhusiano.

Annie ambae ni mhitimu wa masomo ya psychology, anampa kazi Liam ktk kitengo chake Cha kuhifadhi pesa. Katika mahusiano Yao, Liam anawapa taarifa FBI kuhusiana na wizi wake ili aepukane na kesi ya jinai.
Wakala wa FBI Agent Sam anawatuma wasaidiz wake wawili kuchunguza suala hilo,Liam anawaelekeza sahemu alipohifadhi pesa lkn mmoja ya wale FBI anamshawishi mwenzake kuzihifadhi hizo pesa sehem nyingine.

Baada ya kuziiba na kuzihifadhi sehemu nyingine hizo pesa, wale Askari wanarudi kwenye Hoteli anayoishi Liam na kumtolea bastola kuwa ana fedha nyingine nyingi kazificha. Hata ivyo,bosi wao anawasili hapo, na katika majibizano mmoja wa askar anamuua bosi wake, Liam anafanikiwa kutoroka na Dem wake.

Liam anamwambia Annie Kila kitu na anamshawishi atoroke akihofia usalama wake, lkn Annie anarudi kwenye kitengo Cha kuhifadhi pesa kupata ushahidi wa kamera ambazo ni kweli zinaonyesha askari wale wakiiba zile pesa, isivyo bahati kabla hajaondoka anakutwa na wale Askari, anapigwa na kupoteza faham ili kupoteza ushahidi.

Liam alifanikiwa kumpeleka hospitali lkn anaingia kwenye pambano dhidi ya polisi na anafanikiwa kuwatoroka. Wale askari wakiwa wanajua yule Dem ana ushahidi wa kamera wakapanga kwenda kumuua hukohuko hospitali jambo hilo linakua gumu kwani rafiki wa bosi wao alikuja kumuona Annie ili nae ajue chanzo Cha kifo Cha rafiki yake...............KIMBEMBE!!!

Je, hatma ya Liam Neeson itakuwaje, na vipi kuhusu Hawa askari ambao wanataka kumbambikizia kesi mzee wetu watafanikiwa?

Itafute hi "HONEST THIEF" mojawapo ya kazi Bora kabisa kutoka kwa Liam Neeson.

HYPNOTICWakati naiangalia hii muvi nikawa naikumbuka muvi ya Inception ya mtu mzima Christopher Nolan iliyoigizwa na Leo...
21/02/2025

HYPNOTIC

Wakati naiangalia hii muvi nikawa naikumbuka muvi ya Inception ya mtu mzima Christopher Nolan iliyoigizwa na Leonardo DiCaprio. Ilikuwa ni muvi ngumu sana kuielewa, unapoiangalia unaweza kutoka kapa ila ni muvi bora sana ambayo ina rate ya 8.5.

Sasa humu bwana sijui nikuambieje ili uelewe. Ila stori fupi ni kwamba kuna polisi mmoja ambaye alikuwa na mtoto wake, bahati mbaya mtoto huyo alipotea kwenye mazingira ya kutatanisha, na inasemekana kwamba tayari ameuawa mahali.

Sasa baba anahisi kwamba mtoto wake yupo hai hivyo anaanza kumtafuta. Ukiachana na yeye, pia kuna mtu anamtaka mtoto wake, anamtafuta kila kona. Kwa nini huyu jamaa naye anamtaka mtoto wake? Huyu jamaa ni nani?

Huyo mchizi ndiyo wanaofanya hii kitu ya kuitwa Hypnotic. Hii ni nini? Ni ile hali ya kusoma mawazo ya mtu na kumfanya afanye kile unachokitaka wewe. Nahisi hujanielewa, twende sawa.

Mfano nimekukuta umekaa na washikaji zako, halafu moyoni nazungumza na akili yako, naiambia hebu mkate kibao huyo jamaa wa kushoto, na wewe bila kuuliza unamkata kofi huyo jamaa k**a nilivyozungumza nawe kwenye mind yako.

Nadhani umenielewa. Sasa nenda kaicheki! Bonge moja la muvi.

Umewahi kuitazama  Muvi iitwayo  300?Kwenye hii dunia kuna watu waliitwa Spartans, hao walikuwa wazee wa vita, yaani wal...
20/02/2025

Umewahi kuitazama Muvi iitwayo 300?

Kwenye hii dunia kuna watu waliitwa Spartans, hao walikuwa wazee wa vita, yaani walikuwa hatari kwenye uwanja wa vita k**a nini.

K**a umewahi kuitazama 300 Sasa wale watu ndiyo Spartans, kwanza walipenda vita na walivijua vilivyo.

Wakati Leonidas alipokuwa na jeshi la watu 8000 alikuwa akijiandaa kupigana na wanajeshi 150,000 wa Persia. Kwa busara tu mfalme wa Persia, Xerxi alimtumia ujumbe Leonids na kumwambia alisalimishe jeshi lakini mwanaume huyo akamjibu: “Njoo ulichukue.”

Wakati baba yake Alexander The Great, Mfalme Philip alipoichukua Ugiriki, alibakisha mji mmoja wa Sparta, akatuma ujumbe kwao uliosomeka: “K**a nikiivamia Leconia, nitauharibu mji na kuwamaliza wote na hamtokuwa na nguvu tena.”

Spartans wakajibu kwa neno moja tu...KAMA.

Katika kipindi cha vita iliyojulikana k**a Thermopylae kati ya Spartans na Persian, majamaa wakamtumia ujumbe Dienekes walikuwa na mishale mingi ambayo ikirushwa kwa pamoja inaweza hata kuufunika mwanga wa jua.

Akasema: “Waambie wasijali, hiyo vita tutapigana nao usiku.”

Majamaa walikuwa wababe haswa.

Tuingazie Bongo Muvi Bongo Movie imekuwa na mchango mkubwa katika jamii ya Kitanzania, lakini pia imekumbwa na changamot...
16/02/2025

Tuingazie Bongo Muvi

Bongo Movie imekuwa na mchango mkubwa katika jamii ya Kitanzania, lakini pia imekumbwa na changamoto mbalimbali kwa wakati huu.

Mabadiliko ya zama hizi za sayansi na teknologia,utandawazi na urahisi wa kupata maarifa umechangia sana kuporomoka kwa Bongo muvi! Zamani haikuwa rahisi kupata muvi na series za kigeni bila kwenda banda la video lakini kwa sasa unapata kila kitu kiganjani mwako. Hii imechamgia kuuwa soko la filamu za kitanzania kwa kiasi kikubwa.
Pamoja na hayo nikiri ukweli kwamba sanaa ya kitanzania imekuwa na Mchango Chanya kwenye jamii yetu kwa mfano
Elimu kwa Jamii – Baadhi ya filamu za Kibongo zimekuwa na mchango mkubwa katika kutoa elimu kwa jamii. Mfano, filamu k**a PIGO inatoa elimu kuhusu saratani ya shingo ya kizazi na umuhimu wa afya bora. Kwa upande wa ajira na Uchumi – Tasnia ya filamu imewapa ajira maelfu ya vijana, kuanzia waigizaji, waandaaji wa filamu, wapambaji, hadi watayarishaji wa muziki wa filamu lakini pia imekuwa Utambulisho wa Utamaduni wa kitanzania,Filamu nyingi za Bongo Movie huakisi maisha halisi ya Watanzania, ikiwemo mila, desturi na changamoto za kijamii, hivyo kusaidia kuhifadhi utamaduni wa taifa bila kusahau Burudani na Starehe kwani Filamu hizi zimekuwa burudani kwa watu wa rika zote, zikiwa sehemu ya maisha ya kila siku na kuleta faraja kwa wengi.

Pamoja na mchango huo chanya pia kumekuwa na mchango hasi k**a vile
Kueneza Maisha Bandia – Filamu nyingi zinaonyesha maisha ya kifahari yasiyoendana na hali halisi ya Watanzania, jambo linaloweza kuathiri vijana kwa kuwapa matarajio yasiyo halisi.

Kushuka kwa Ubora wa Filamu – Ukosefu wa hadithi zenye maudhui mazito na waigizaji wenye weledi umesababisha tasnia hii kupungua thamani sokoni. Watazamaji wengi wameanza kupendelea filamu za nje zenye viwango vya juu zaidi.

Kuvunjika kwa Maadili – Baadhi ya filamu zinalalamikiwa kwa kuhamasisha mmomonyoko wa maadili, ikiwemo mavazi yasiyozingatia utamaduni wa Kitanzania na tabia zisizofaa kwa vijana.

Soko Duni la Filamu – Kutokana na ongezeko la simu janja na mitandao ya kijamii, waigizaji wengi wanatumia njia rahisi za kujipatia umaarufu, hali inayoathiri sana soko la filamu za Kibongo.

Una maoni gani kuhusu andiko hili? Toa maoni yako!

DMX ANGEKUWA RAPA WA KWANZA KUWA BILIONEAHayo yalikuwa maneno ya mkewe, Tashera Simmons. Mwanamke huyo anasema:“Nakumbuk...
15/02/2025

DMX ANGEKUWA RAPA WA KWANZA KUWA BILIONEA

Hayo yalikuwa maneno ya mkewe, Tashera Simmons. Mwanamke huyo anasema:

“Nakumbuka kipindi nilipokuwa naangalia akaunti yetu ya benki, sifuri zilikuwa hazikomi, mume wangu alikuwa anatengeneza dola milioni 10 kwa kila muvi aliyoigiza na alikuwa anatengeneza milioni moja ama zaidi kwa kila shoo aliyokuwa akiifanya. Alipokuwa akienda tour, pesa alizokuwa akirudi nazo zilikuwa nyingi sana.”

Mwanamke huyo anasema DMX hakuwa na midset ya biashara, ndiyo alikuwa anatengeneza pesa nyingi lakini jamaa hakuwekeza.

Anasema kuna kipindi alifuatwa na kuambiwa atoe milioni kadhaa kwa ajili ya kuwekeza katika ukumbi wa Barclays Center ambapo hapo hufanyika michezo mbalimbali na ndipo muda huohuo naye Jay Z aliiona hiyo opportunity na kuambiwa, akatoa mamilioni, akawekeza.

DMX hakutaka kuwekeza. Anasema:

“Sitoweza kusahau. Walimpigia simu na kumwambia Jay Z amekubali kuweka mamilioni kwa nini na wewe usiweke kwenye hii project? Bahati mbaya hakuwa na maono ya biashara, hakujua k**a baadaye itakuja kuingiza mamilioni, alikataa kataka.

“DMX alitumia pesa zake nyingi kwa ajili ya wengine. Alipokuwa akisikia fulani amefiwa, basi alikuwa mstari wa mbele kushughulikia mazishi yote, tulipokuwa tukienda vacation alikodi hoteli nzima na kutumia kiasi cha dola 150,000 kwa siku.”

(Kibongobongo ni zaidi ya milioni 380)

Pamoja na kuuza mambilioni ya albamu na kuingiza pesa nyingi lakini uchumi wa jamaa ukaja kuyumba, akawa na madeni mengi na kufilisika kabisa na baadaye kufungwa gerezani kwa kosa la kukwepa kulipa kodi ambapo alitakiwa kulipia dola milioni 2.

Alipofariki dunia mwaka 2021 DMX hakuacha chochote nyuma yake zaidi ya madeni makubwa. Hilo lilikuwa anguko kubwa la msanii ambaye aliwahi kuwa juu kabisa kimuiziki miaka ya 2000.

Interview hiyo kwa mke huyo ilifanywa na mwandishi Carlos King.

Mzigo huo hapo.Unaitwa Moment of Contact.Mzigo ni documentary moja ya kibabe sana iliyotoka mwaka 2022 ambayo ilipigwa n...
14/02/2025

Mzigo huo hapo.
Unaitwa Moment of Contact.
Mzigo ni documentary moja ya kibabe sana iliyotoka mwaka 2022 ambayo ilipigwa na jamaa wa kuitwa James Fox.
Hii documentary imefanyikia huko America ya Kusini nchi moja ya kuitwa Brazil.

Imetoka mwaka huo ilamchongo huu ulifanyika mwaka 1996. mahojiano ya raia mbalimbali kuhusu Aliens, waliowashuhudia kwa macho yao walizungumza sana humo, k**a unataka kujua mengi kuhusu hawa viumbe, nikupe nafasi tu ukautafute huu mzigo.

Umepachikwa kule Watch So Much, k**a vipi kaupakue.

Umeitazama  SNOWFALL?Nimeanza kuifuatilia hii series ya Snowfall, ni moja ya series kali sana lakini unatakiwa usiwe na ...
13/02/2025

Umeitazama SNOWFALL?

Nimeanza kuifuatilia hii series ya Snowfall, ni moja ya series kali sana lakini unatakiwa usiwe na presha unapoanza kuiangalia, na imenifundisha baadhi ya mambo.

1. Unatakiwa kujua unataka nini, huwezi kukurupuka kufanya biashara huku ukiwa hujui unataka nini.

2. Unapoanza kufanya biashara na mtu fulani, hata k**a yeye anakuuzia bidhaa, jitahidi sana na wewe utengeneze bidhaa zako, yaani k**a kutafuta mzigo sehemu nyingine, usitake kuchukua mzigo sehemu moja.

3. Unapoanza kutengeneza njia ambayo unaamini ina mafanikio, usimsikilize mtu mwingine, hata k**a ni mama yako atakwambia hiyo njia si sahihi, k**a unaamini ni sahihi, nenda nayo. Utakapohustle, utahustle peke yako tu.

4. Chagua kampani ya kufanya nayo kazi pamoja, usichukue rafiki ambaye unaona kabisa hawezi kusapoti hiki ninachokifanya. Ukiona rafiki hasapoti, mteme, katafute wengine unaoona nitapambana nao bega kwa bega.

5. Hutakiwi kuwa na huruma hata kidogo. Biashara ili isimame unatakiwa kuwa na roho mbaya.

6. Usiwe mtu wa kupaniki kwenye kufanya maamuzi, calm down, think halafu fanya jambo. Kamwe usifanye maamuziki ukiwa na hasira.

7. Jua ukifeli, umefeli maisha yako na si ya mtu mwingine.

8. Mshirikishe mpenzi wako ajue biashara unayoifanya, mwisho achague kuendelea kubaki na wewe ama ale njia yake.

9. Hata uwe bize vipi, hata uwe unapambana na kukosa muda, jitahidi sana uwe unafanya mapenzi kuirefresh akili yako.

10. Mtu akimess up na biashara yako, mess up na maisha yake.

Address

Dar Es Salaam
Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Muvi Na Burudani posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share